Akothee awasifu single mothers baada ya binti ya Pierra Makena kupata kazi Churchill Show

Pia alimpongeza Ricca kufuatia mafanikio makubwa ya kuandaa kipindi cha TV katika umri mdogo sana.

Muhtasari

•Binti ya DJ Pierra Makena, Ricca Pokot, alichaguliwa kutangaza kipindi cha watoto kwenye msimu mpya wa Churchill Show.

•Bintiye Pierra Makena mwenye umri wa miaka minane alizungumza kuhusu kuchaguliwa kwake kuandaa kipindi cha watoto kwenye Churchill.

Akothee, Pierra Makena na Binti yake Rica Pokot
Image: HISANI

Mwimbaji na mjasiriamali mashuhuri wa Kenya Esther Akoth almaarufu Akothee amewapongeza akina mama wasiokuwa na waume kwa kujenga ujasiri kwa watoto wao.

Hii inafuatia mafanikio ya hivi majuzi ya binti ya DJ Pierra Makena, Ricca Pokot, ambaye alichaguliwa kutangaza kipindi cha watoto kwenye msimu mpya wa Churchill Show.

Huku akimpongeza mcheza santuri Pierra Makena kwa jinsi alivyomlea mtoto wake, Akothee alibainisha kuwa akina mama wasio na waume ni wazuri katika kujenga ujasiri kwa watoto wao. Pia alimpongeza Ricca juu ya mafanikio makubwa ya kuandaa kipindi cha TV katika umri mdogo sana.

“Single mothers hoyeeeeee. Timu iliyoshinda. Tafadhali fuata mtoto wangu, yoooo ujasiri wa mtoto wangu katika kiwango kingine @pierramakenaofficial. Yooooooo hakuna mtu anayeweza kumshinda mama asiye na mume linapokuja suala la kujenga ujasiri wa watoto wake. Nakupenda msichana. Hongera 💕,” Akothee alisema hapa chini video ya Ricca aliyoichapisha.

Katika video ambayo mwimbaji huyo alichapisha, bintiye Pierra Makena mwenye umri wa miaka minane alisikika akizungumza kuhusu kuchaguliwa kwake kuandaa kipindi cha watoto kwenye Churchill.

Kisha akawaomba watumiaji wa mitandao kumfuata kwenye akaunti zake zote za mitandao ya kijamii.

"Kila mtu anashangaa kwa nini nina furaha sana, kwa nini ninaonekana mwenye nguvu. Ni kwa sababu mimi ni mtangazaji wa Kipindi kipya cha Churchill kwenye NTV, na nisingeweza kufanya hivyo bila nyinyi watu,” Rica alisema.

Katika siku za nyuma, DJ Pierra alisema alidhani hangeweza kamwe kumlea binti yake peke yake baada ya kuachana na baba mtoto. Hata hivyo, alishangazwa na jinsi alivyokuwa amefika.