logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kikosi cha MIC Cheque chaomboleza kifo cha mmoja wao

Kikundi hicho kimesimamisha shughuli zake za wiki hii.

image
na Brandon Asiema

Burudani21 October 2024 - 12:22

Muhtasari


  • Timu hiyo pia imearifu kuchukua muda wa wiki moja ili kuomboleza kifo cha mwenzao kikisema kuwa shughuli zao za kawaida zitarejea wiki ijayo

Watengenezaji wa maudhui ya Youtube Mic Cheque podcast wamesitisha shughuli zao za kutengeneza maudhui kwa muda baada ya kifo cha mmoja wa wafanyakazi wake kuaga dunia.

Kupitia ujumbe kwa ukurasa wao wa Instagram, kikundi hicho kimechapisha taarifa hizo za huzuni kikieleza kuwa maudhui ya wiki hii hayatawekwa mtandaoni kupisha maombolezo ya mwenzao aliyefariki.

“Ni kwa mioyo mizito kwamba tunatoa taarifa za kusikitisha. Wiki jana, tulimpoteza mpendwa wetu katika timu ya Mic Cheque Podcast.”  Taarifa ya timu ya podikasti hiyo ilisoma.

Kwenye taarifa, timu ya Mic Cheque iliwashukuru mashabiki wake kwa kuelewa kwao na usaidizi wao wakati wa majonzi.

Timu hiyo pia imetangaza kuchukua muda wa wiki moja ili kuomboleza kifo cha mwenzao kikisema kuwa shughuli zao za kawaida zitarejea wiki ijayo.

“Hakutakuwa na vipindi vipya wiki hii tunapochukua muda kutafakari na kukumbuka. Asante kwa kuwa sehemu ya safari hii nasi. Tunaangazia kurejea wiki lijalo.”   Wanapodikasti hao walisema kupitia ujumbe kwa taarifa yao.

Hata hivyo, watengenezaji maudhui hao hawakuweka wazi jina la mwenzao aliyeaga dunia sawia na kutoa taarifa zaidi ya sababu ya mauti yaliyiotukia wala mipango ya mazishi ya mwendazake.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved