'Mapenzi siyataki tena,'Paula Kajala adai baada ya Rayvanny kupakia picha ya Fayvanny

Muhtasari
  • Rayvanny aliachana na mpenzi wake na mama wa mtoto wake Fahyma mapema mwaka huu 

Rayvanny ni msanii wa Bongo aliyesajiliwa chini ya WCB Wasafi. Yeye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Next Level music.

Rayvanny aliachana na mpenzi wake na mama wa mtoto wake Fahyma mapema mwaka huu .

Alianza kuchumbiana na binti wa muigizaji maarufu Paula Kajala . Paula ni mwanamitindo na mshawishi wa chapa.

Tangu wawili hao waanze kuchumbiana wameonyesha mapenzi  kwenye mitandao ya kijamii huku wakipost kila mmoja akitoa maneno ya mapenzi .

Jana msanii huyo alitumia hadithi zake za Instagram kumpost mpenzi wake wa zamani Fahyma.

Baada ya muda msanii huyo aliichomoa picha hiyo .Saa moja baada ya msanii huyo kufuta picha hiyo Paula Kajala aliacha kumfuata ambayo baadaye ilifuatiwa na Rayvanny na kuaha kumfuata Pala kweye ukurasa wake wa instagram.

Wawili hao ambao hawajafuatana wamewaacha mashabiki wakiulizana iwapo bado wapo pamoja au ni kikitu wa kuutangaza wimbo wake mpya kabisa na Maluma. ?

Kupitia kwenye ukurasa wake kajala, alisemma kwamba ameacha mambo ya mapenzi, na kutia bidii kwenye masomo yake.

"Ngoja nikazane na masomo tuušŸ˜­šŸ˜­ mapenzi siyataki tena jamanišŸ˜© basi nikisema hivi kuna vizabi zabina leo watapika pilau kufurahiašŸ¤£šŸ¤£šŸ¤£," Paula aliandika.

Pia Paula kwenye ukurasa wake mwingine wa instagram siku ya JUmamosi alidai kwama yeye na Rayvanny hawataachana, na kwa wanao ngoja waachane haya basi watangoja sana.

"Mimi kuachana na Rayvanny sio leo wala kesho mpaka Mungu atakapo tutenganisha mpoo?šŸ¤£šŸ¤£šŸ¤£ mtasubiri zaidi ya Jux vizabi nyie mpigwe shoti mfe wale msiopenda mahusiano yangu na ray."