Wanamitandao wasifia urembo wa mwanawe mwanasosholaiti Vera Sidika

Muhtasari
  • Wanamitandao wasifia urembo wa mwanawe mwanasosholaiti Vera Sidika
Image: INSTAGRAM// VERA SIDIKA

Mwanasosholaiti Vera Sidika Jumatatu kupitia kwenye ukurasa wake wa  instagram alitambulisha picha ya mwanawe kwa mara ya kwanza.

Vera wakiwa na mume wake, Brown Mauzo walionyesha  sura ya mwanao kwa mara ya kwanza huku Vera  akionyesha furaha kubwa kwa maandishi yaliyoambaatana na  picha ile ya kifungua mimba wao

Ikumbukwe wanamitandao wamekuwa wakitoa maneno mbalimbali huku wakitaka kujua mtoto Asia anafanana na nani baina ya wazazi hao wawili.

Sidika anajulikana sana kwa maisha yake ya kutatanisha. Aliwahi kuibuka madai kwamba ametumia mamilioni ya pesa kubadilisha  mwonekano wake wa ngozi huku wanamtandao wakitabiri mtoto  wake atakuwa  na rangi ya asili .

Wanamitandao hawakubaki nyuma kutoa kauli zao ambazo zilikuwa kinyume na matarajio kwani mtoto huyo alikuwa amependeza ajabu huku wengine wakisema mtoto amechukua sura ya  baba yake, Brown Mauzo

Baadhi za ujumbe ya wanamtandao ni kama;