Vitu ambazo Erick alionyesha kwenye kanda hio zilikuwa simu dogo ya 'mulika mwizi' , kifaa cha kinyolea na chupi ya mwanamke.
Mchekeshaji Eric Omondi kupitia kanda ya video amedai ako na vitu mwanamuziki wa kikundi cha Sauti Sol, Bien alipoteza katika tamasha ya Konshens iliyofanyika Carnivore mnamo Desemba 31 .
Kupitia kwa video aliyopakia Instagram, Omondi alitaja na kuonyesha vitu kadhaa ambazo anadai ni za msanii huyo. Cha kushangaza ni kuwa vitu zenye mcheshi huyo alionyesha vitu zaidi ya zile Bien alitaja kapoteza.
Mcheshi Eric alidai kwa simu ambayo anadai alichukua kutoka kwa Bien hakukuwa na 'voice notes' alizotaja mwanamuziki huyo katika tangazo lake.
"Kama umeishiwa na mawazo umekosa maangoma, umepanic! usinitumie kusema album yako imeibiwa . Album gani imeibwa? ..hizo vitu niko nazo zote,. ngoma zinawekwa kwa kompyuta kwa studio si kwenye simu. kama umeishiwa na mawazo .. acha woga, tafuta mtu akuandikie mangoma. kujia vitu zako Bwana," alisema.
Vitu ambazo Erick alionyesha kwenye kanda hio zilikuwa simu dogo ya 'mulika mwizi' , kifaa cha kinyolea na chupi ya mwanamke.
Bien alipotangaza kwamba alipoteza vitu vyake vya thamani katika tamasha ya kufunga mwaka Carnivore ambayo ilihudhuriwa na mwimbaji wa Jamaika Konshens na kutoa zawadi ya Ksh 50,000 kwa yeyote atakeyezipata vitu hizo.