Mama mtoto wa Davido avunja kimya

Muhtasari

•Sophie Momodu, ambaye ni mama mzazi wa mtoto wa kwanza wa msanii maruufu nchini Nigeria, Davido

•Sophia Momodu alisema ashamaliza kukaa kimya kuhusu kile wanamitandao  wanakichapisha kumhusu  yeye

Msanii DAVIDO
Msanii DAVIDO
Image: INSTAGRAM// DAVIDO

Mpenzi wa zamani wa msanii Davido, Sophie Momodu amejitokeza na kueleza bayana kuhusu watu wanaomsumbua mtandaoni kwa kucheza na hisia zake 

Sophie Momodu, ambaye ni mama mzazi wa mtoto wa kwanza wa msanii maruufu nchini Nigeria, Davido. Kupitia ukurasa wake wa Instagram alitokwa na chozi huku akieleza kero wanamitandao wamekuwa wakieneza uvumi kwa mitandao kwa mambo wasioyajua.

Sophia Momodu alisema ashamaliza kukaa kimya kuhusu kile wanamitandao  wanakichapisha kumhusu  yeye.Alionyesha kukasirishwa na kundi la watu linalomuandama kwa kuonekana kumuunga mkono baba ya mtoto wake 

Akizungumza kuhusu tuhuma za kuwa na marumbano na mwanamke  anayesemekana ni mama wa mtoto wa pili wa  Davido. kwa mujibu wake alidai. alitumia miaka sita iliyopita kupambana na watu mitandaoni ambao hawajawi kuona lolote jema kumhusu yeye.

"Imekuwa miaka 6 ya kumtukana Sophia. imetosha. Niacheni," alisema 

Aidha, alisema anachojaribu kufanya ni kumlea binti yake kuhakikisha ana husiano mwema  na babake yake. alitimiza kwa kusema mwaka huu mpya wa 2022, hutofumbia macho yeyote atayeeneza uvumi juu yake hasa utakaohusisha  mzazi mwenza.

 .