"Naomba Kolabo" Makabila amwambia Nandy

Muhtasari

• Staa wa Bongo wa mtindo wa Singeli, Dulla Makabila amejitokeza wazi na kumweleza The African Princes  almaarufu Nandy kwamba anataka wafanye Kolabo.

The Africa princess 'Nandy'
The Africa princess 'Nandy'
Image: Facebook/ Nandy

Staa wa Bongo wa mtindo wa Singeli, Dulla Makabila amejitokeza wazi na kumweleza The African Princes almaarufu Nandy kwamba anataka Kolabo naye.

Dulla, ambaye alipakia video  kwenye ukarasa wake wa Instagram, akiwa kwenye tamasha za  kufunga mwaka Nandy, alieleza anatamani kufanikisha malengo yake  kufanya kazi  ya muziki pamoja na Nandy.

"Hongera Sana Mwanangu Umeua Mnoo Naamini Kwenye Uwezo Wako  Kuna Haja ya Kufanya Kitu Naomba simamia    Hili Mashabiki Wa Singeli Wamependezewa Na Anachokifanya Mrs Billnass

Nandy, ambaye ni  msanii kutoka nchi ya Tanzania, vile vile muigizaji kwenye mojawapo ya kipindi sifiki  nchini Tanzania alionekana kupendezwa na pendekezo hilo la  Makabila. Alitumia sehemu ya maoni ya Makabali  kuonyesha ni pendekezo nzuri huku  akitumia alama ya moto kuthibitisha ameona.

Kilichosalia ni kwa Meneja wanaosimamia kazi ya Nandy kupanda wakati wa kutimiza pendekezo  hilo la Mwanamuziki maarufu wa Singeli, Makabali