Msanii tajika katika kanda la Afrika Mashariki Diamond Platnumz amezuru nchi ya Nigeria, Lagos ambapo alionekana akiwa amepewa ulinzi mkali achia mbali ulinzi marais wa Afrika upewa.
Kupitia ukurasa wake wa insta story ameweka video ambayo anaonekana akitoka kwa gari lake huku walinzi wake wakiwa tayari kumpokea.
Diamond alikuwa pamoja na msanii wa lebo yake ya Wasafi record Mbosso huku wafuasi wake wakitabiri kuwa wanangoja kibao kipya kutokana na safari hiyo.
Diamond ambaye pia anamiliki kituo cha habarini nchini Tanzania amekuwa akizuru nchi tofauti tofauti kwa minajili ya kazi yake ya muziki
Hivi majuzi habari zimekuwa zikienea kwenye mtandao ya kijamii kwamba Diamond ambaye mashabiki wake upenda kumuita, wanamahusiano na Zuchu.
Zuchu alijitokeza wazi wazi na kukana madai hayo, huku akisema kwamba yuko 'single'.