Diamond apewa ulinzi mkali nchini Nigeria Lagos

Muhtasari
  • Diamond Platnumz  amezuru nchi ya Nigeria, Lagos ambapo alionekana akiwa amepewa ulinzi mkali achia mbali ulinzi marais wa Afrika upewa
  • Hivi majuzi habari zimekuwa zikienea kwenye  mtandao ya kijamii kwamba Diamond ambaye mashabiki wake upenda kumuita, wanamahusiano na  Zuchu. 

 

Diamond Platnumz
Diamond Platnumz
Image: instagram/Diamond platnumz

Msanii tajika katika  kanda la Afrika Mashariki  Diamond Platnumz  amezuru nchi ya Nigeria, Lagos ambapo alionekana akiwa amepewa ulinzi mkali achia mbali ulinzi marais wa Afrika upewa.

Kupitia ukurasa wake wa  insta story ameweka video ambayo anaonekana akitoka kwa gari lake huku walinzi wake wakiwa tayari kumpokea.

Diamond alikuwa pamoja na msanii wa lebo yake ya Wasafi record Mbosso huku wafuasi wake wakitabiri kuwa wanangoja kibao kipya kutokana na safari hiyo.

Diamond ambaye pia anamiliki kituo cha habarini nchini Tanzania amekuwa akizuru nchi tofauti tofauti kwa minajili ya kazi  yake ya muziki 

Hivi majuzi habari zimekuwa zikienea kwenye  mtandao ya kijamii kwamba Diamond ambaye mashabiki wake upenda kumuita, wanamahusiano na  Zuchu. 

Zuchu alijitokeza wazi wazi na kukana madai hayo, huku akisema kwamba yuko 'single'.