•Briana, ameeleza eneo ambalo walikutana mara kwanza na mwanamuziki huyo na wakazama kwenye penzi
•Kulingana na Briana , walipatana na harmonize mara ya kwanza kwenye eneo la burudani nchini Sydney na wakaanza kuzungumza lakini mwaka 2021 ndio alizuru nchi ya Tanzania.
Mpenzi wa Harmonize anayetambulika kama Briana, ameeleza eneo ambalo walikutana mara kwanza na mwanamuziki huyo na wakazama kwenye penzi.
Kulingana na Briana , walipatana na harmonize mara ya kwanza kwenye eneo la burudani nchini Sydney na wakaanza kuzungumza lakini mwaka 2021 ndio alizuru nchi ya Tanzania.
Harmonize mwaka jana alijitokeza na kueleza kiini cha kukosana na wapenzi wake, huku akidai mahusiano yake mengi huvunjwa na aliyekuwa mwajiri wake wazamani Diamond Platnumz.
Hivi majuzi harmonize amekuwa akionekana na Briana kwenye tamasha mbalimbali huku mashabiki wake wakiMpongeza kwa mahusiano yake na mzungu.
Harmonize ambaye aligura lebo ya Wasafi inayomilikiwa na Diamond Platnumz, na kuanzisha lebo yake ya Konde gang siku za hivi majuzi lebo yake imefikiana na country Boy kuondoka kwa kile walisema ni msanii huyo alikatisha muktaba wake.