• Diamond Platnumz alizungumzia kiwango cha ubora wa Ravyaan na kuwapongeza wote waliomsaidia kumsajili kwenye lebo yake.
• Kilichosalia kwa wafuasi wa Ravyaan nikuona akitangaza siku rasmi ya kuaga Wasafi kama alivyofanya Harmonize.
Siku chache zilizopita kumekuwa na uvumi kuhusu hatma ya mwanamuziki Ryvanny katika lebo ya Wasafi.
Wiki jana Mkubwa Fella akizungumza na kituo kimoja cha radio nchini Tanzania akigusia jambo hilo ingawa hakutaja jina la msanii aliyekuwa ananjama ya kuondoka Wasafi.
Alisema, aliuliza Diamond kuhusu msanii anayetaka kuondoka na Diamond akamjibu kuwa... "muziki wa Bongo flava naujua na anayetaka kuondoka naondoke".
Wikendi hii kwenye uzinduzi wa lebo ya Ravyaan, Diamond Platnumz alizungumzia kiwango cha ubora wa Ravyaan na kuwapongeza wote waliomsaidia kumsajili kwenye lebo yake.
Diamond ambaye alikuwa amevaa suti ambayo inasawiana na Ravyaan alieleza safari ya Rayvanny tangu wamsajili na mambo aliyoafikia akiwa kwenye lebo hiyo.
"kwanza niwashukuru wote, najua kuna mambo mengi yanaendelea duniani lakini mwenyezi Mungu katuponya..kwa upande wangu kabla sijaenda mbali na washukuru Babu Talle na Madihi kwa sababu chimbuko la Ravyaan lilikuwa pale. Lakini baada ya kukutana naye nikaona ana kipaji na kwa kipindi kile nilikuwa naanzisha lebo yangu ya Wasafi, tuliongea na wakubwa wake tukawaomba watupe Ravyaan," alisema Diamond
Alieleza wazi kwamba Rayvanny tangu wamsajili amekuwa akionyesha ubora wake kwa kila kazi yake.
"kuanza kufanya kazi na Ravyaaan alikuwa akikua kwa kasi,, hadi kufikia hapa, Ravyaan Mimi nakupongeza sana kwa sababu sio tu mimi ila Wasafi nzima kwa kuifanya itambulike zaidi,"
Kilichosalia kwa wafuasi wa Ravyaan nikuona akitangaza siku rasmi ya kuaga Wasafi kama alivyofanya Harmonize.