•Harmonize alichapisha video fupi iliyokuwa ikicheza wimbo mpya wa Alikiba unaoitwa ‘Utu’ huku akiambatinisha na ujumbe kwamba siku ya kuvisha pete mpenzi wake lazima King Kiba atumbuize mashabiki wake.
Mwanamuziki Maarufu nchini Tanzania Harmonize ameonyesha heshima kwa mwanamuziki mwenzake wa Bongo Flava Alikiba kwa kumpongeza kwa kazi nzuri anayofanya kwenye tasnia ya Muziki wa Bongo.
Kupitia ukurasa wake Wa instagram, Harmonize alichapisha video fupi iliyokuwa ikicheza wimbo mpya wa Alikiba unaoitwa ‘Utu’ huku akiambatinisha na ujumbe kwamba siku ya kuvisha pete mpenzi wake lazima King Kiba atumbuize mashabiki wake.
“Mtu amwambie mkongwe, mfalme Alikiba lazima aimbe kwenye usiku wa kumvisha pete mchumba wangu, huu muziki mzuri sana,” Harmonize aliandika.
Hivi majuzi wanamuziki hao walionekana wakisafiri kwa ndege moja, jambo ambalo wanamitandao walilijadili kwa wiki kadhaa.
Ikikumbukwa wasanii waliosajiliwa na wasafi Record hawana mkabala mzuri na Ali Kiba.
Swali ambalo wengi wanajiuliza kwa sasa ni kwa nni Harmonize amekuwa na mkabala mwema na Ali kiba ikikumbukwa wakati alikuwa Wasafi hawakuwa wanazungumza.