•Msanii Arrow Bwoy alieleza kuwa mtangazaji Jalango aliomba msamaha kufuatia maneno aliyotoa mwezi jana kuhusu familia yake
•Alikuwa anahojiwa na kituo kimoja cha radio nchini Kenya ambapo alieleza kuwa Jalang’o alipita mipaka wakati alikuwa akizungumzia suala la mahusiano baina yake na Nadia Mukami
Msanii Arrow Bwoy alieleza kuwa mtangazaji Jalang''o aliomba msamaha kufuatia maneno aliyotoa mwezi jana kuhusu familia yake.
Arrow, ambaye alikuwa anahojiwa na kituo kimoja cha radio nchini Kenya, alieleza kuwa Jalang'o alipita mipaka ya kuongea wakati alikuwa akizungumza kuhusu mahusiano baina yake na Nadia Mukami.
“Jalas ni rafiki yangu, ni mtu ambaye ameniunga mkono tangu siku ya kwanza, ni jamaa mzuri sana, bado tungali tunaongea lakini siku hio alivuka mipaka. Hakuna shida yoyote kati yetu,alinitumia ujumbe akiomba msamaha, na mimi napenda kusamehe nilimsamehe," alisema Arrow Bwoy.
Ikumbukwe Arrow Bwoy alijitokeza na kumkashifu Jalang’o na kumuonya dhidi ya kuongea mambo yake ya familia.
Vilevile, Nadia Mukami alionyesha ghadhabu yake kupitia ukurusa wake wa Instagram kuhusu kitendo cha Jalang'o huku akitaja Arrow Bwoy kuwa jamaa ambaye hapendi kuongea mambo yanayohusu familia.