Aliwapa watu 'block' kwenye simu yangu- Aliyekuwa mpenzi wake Amber Ray atoa sababu ya kuachana naye

Muhtasari
  • Aliyekuwa mpenzi wake Amber Ray atoa sababu ya kuachana naye
Amber Ray
Amber Ray
Image: INSTAGRAM

Mpenzi wa zamani wa Amber Ray nyota wa mpira wa vikapu kutoka Sierra Leonia amefunguka kuhusu uhusiano wake mfupi na mwanasosholaiti huyo.

IB Kabba alieleza kwa kina safari yake ya kuendelea baada ya penzi la kimbunga na Amber Ray ambalo liliisha kabla halijaanza.

"Ninahisi kama nilienda huko kwa ajili yako halafu ghafla hutaki kuondoka, nilichukua simu yake, nikaishia kumrudishia simu, Najua nilichofanya kilikuwa kibaya lakini nilitaka kurekebisha mambo."

Kabba aliongeza, "Nilituma video hiyo kwa marafiki zangu, kama ushahidi kwamba sikuwahi kumpiga Amber Ray. Siwezi kumpiga mwanamke."

Alipoulizwa kwa nini waliachana, Kabba alisema;

"Ni mambo ya kawaida ya uhusiano ambayo hutokea. Uhusiano unafanya kazi kwa njia zote mbili na ninyi nyote mnapaswa kuufanyia kazi. Ikiwa unafanya kitu ambacho si sahihi, basi, ni kama, ' Nataka kuwa na udhibiti wa maisha yao."

Aliendelea, "Amepindishwa kila kitu, kwanini nitake kudhibiti maisha yake? Alikuwa akitumia simu yangu na ku-block watu kwenye Instagram na sijawahi kuingia kwenye simu yake. Nilichokuwa najaribu kujenga na alichokuwa anajaribu kukifanya. ujenzi ulikuwa tofauti. Haikufaulu."

Alibainisha, "Jambo moja ambalo ningependa kusema ni kwamba sitawahi kumpiga mwanamke."

“Bado ninampenda lakini kila mtu ameendelea. Sikuchukua muda kujua amber Ray ni nani. Sikuzote alikuwa akiniambia nisikilize ninachosikia kumhusu au kusoma kumhusu.”

Kabba alisema walikuwa wamekutana katika mkahawa mmoja jijini Nairobi.

“Rafiki fulani alinitambulisha kwake huko Mialle, kisha tukashiriki waasiliani na kuanza kuzungumza.”

Alisema atachumbiana na mwanamke wa Kenya.

"Kwa sababu tu mtu alinikosea, haimaanishi kuwa wanawake wote wa Kenya ni wabaya."