logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wachana na watoto wangu nilikuachia Jimal-Amira amshambulia Amber Ray

Zaidi ya yote Amira alimuonya Amber dhidi ya kuwa na uhusiano wa na wanawe

image

Burudani28 June 2022 - 11:00

Muhtasari


  • Haya basi tunapofikiria kwamba vita vyao vimefika kikomo,au vimekwisha mambo yanabadilika na wawili hao kuanzisha vita tena

Sio siri wala habari za kushangaza kwamba mwanasosholaiti ndiye sababu ya mwanabiashara Jimal na mkewe Amira kuachana.

Haya basi tunapofikiria kwamba vita vyao vimefika kikomo,au vimekwisha mambo yanabadilika na wawili hao kuanzisha vita tena.

Kupitia kwenye ukurasa wa instagram wa Amira amemuonya Amber Ray dhidi ya kuingilia katika maisha ya watoto wwake.

Kulingana na Amira wikendi iliyopita hakuwa nyumbani, na aliporejea mwanawe alimwambia kwamba Amber Ray alikuwa anamuita wapige picha pamoja, alipotembelea makazi ambayo Amira anaishi.

Zaidi ya yote Amira alimuonya Amber dhidi ya kuwa na uhusiano wa na wanawe, na kumwambia kwamba alimuachia Jimal.

"Mtu amwambie Amber Ray wakati mwingine akija Yamin asivuke mipaka, nilipokuwa siyuko wikendi iliyopita alishinda kumuita mwanangu Shamir, ambaye alikuwa anacheza aende wapige picha pamoja

Aliniambia haya niliporudi nyumbani, sikiza kaa mbali na watoto wangu, nilikuachia Jamal inapokuja kwa watoto wangu tutakosana na tutaona damu," Aliandiika Amira.

Amber Ray hajajitokeza kukana au kukubali madai ya Amira.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved