Wanaume wa Tanzania sio wa kujivunia-Baby mama wake Aslay asema

Muhtasari
  • Tessy alikiri kwamba Aslay amekuwa akimsaidia mwanawe na wala hajawahi mkana mtoto wake

Mama wa mtoto wa msanii Aslay,Tessy akiwa kwenye mahojiano amekiri kwamba amewahi chumbiana na mwanamume ambaye alikuwa kwa ndoa.

Huku akizungumzia hayo Tessy amesema kwamba wanaume kutoka Tanzania sio wa kujivunia nao.

"Nimechumbiana na mwanamume aliyeooa hapo awali. Wanaume wa kitanzania sio wanaume unaweza kujivunia kujionyesha. Sikujua mwanzoni. Aliniambia baadaye kwa sababu alifikiri akiniambia nitamtupa. Hiyo ndiyo ilikuwa sababu mojawapo tuliyoachana. Niliondoka baada ya kujua. Iliumiza hisia zangu kwa sababu nilikuwa nampenda. Nilijiuliza ni siri gani nyingine anazohifadhi."

Tessy alikiri kwamba Aslay amekuwa akimsaidia mwanawe na wala hajawahi mkana mtoto wake.

Tessy anasema kwa sasa yuko single;

“Mahusiano yanaumiza na kumrudisha mtu nyuma, mimi nina moyo mwepesi sana na ni mwaminifu sana kwa watu, lakini wanaume wa Kitanzania sio waaminifu, wanaume wote niliotoka nao kimapenzi wanajua sijawahi kuwacheat, sijawahi kukaa kwenye mahusiano. kwa sababu hivi ndivyo wanaume walivyo."