logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Mwanaume akiku'cheat, usimuache bali m'cheat pia' - Muigizaji wa kike ashauri kina dada (video)

Akijibu, muigizaji alisema; "Nitachepuka."

image
na Davis Ojiambo

Burudani03 February 2024 - 08:32

Muhtasari


  • • Kwa hiyo mhojiwa alimuuliza Laide Bakare “Kwa hiyo mwanaume akikusaliti kimapenzi utamsaliti tena?
  • • Akijibu, muigizaji alisema; "Nitachepuka."
Muigizaji Laide Bakare.

Mwigizaji maarufu wa Nollywood Laide Bakare amezua hisia miongoni mwa watumiaji wa mtandao kufuatia madai yake ya hivi majuzi kuhusu wanaume wanaochepuka katika ndoa zao.

Laide Bakare ambaye alizua uvumi wa ndoa ya 3 wiki zilizopita anawaambia wanawake kwamba ikiwa wanaume wao watawasaliti kimapenzi, wanapaswa kuwasaliti pia, na si kuwaacha au kuvunja mahusiano.

Akiongea zaidi, Laide Bakare alifichua kuwa badala ya mwanamke kuvunja ndoa yake kwa sababu ya mwanamume kutokuwa mwaminifu, anapaswa kusalia kwenye ndoa na kumchepukia mumewe na mwingine.

Akitoa taarifa kulingana na uzoefu wake, Laide Bakare ambaye ana watoto watatu kutoka kwa zake mbili za awali anathibitisha kuwa wanaume wote huchepuka.

Laide Bakare zaidi anawaambia wanawake kufanya hivyo kwa viwango vyote vya ukomavu wanapojaribu kuwachepukia wanaume wao.

Kwa maneno yake; "Wanaume wote wanachepuka, wakati anachepuka ningesema usiondoke lakini unaweza kuchepuka, lakini lazima ufanye kwa viwango vyote vya ukomavu."

Kwa hiyo mhojiwa alimuuliza Laide Bakare “Kwa hiyo mwanaume akikusaliti kimapenzi utamsaliti tena?

Akijibu, muigizaji alisema; "Nitachepuka."

Tazama video hapa chini;


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved