logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wakenya wenye tattoo wafungiwa nje katika usajili wa kujiunga na Huduma ya Kitaifa ya Vijana

Shughuli ya uajiri wa NYS, ilianza Jumatatu, na inatafuta kuajiri angalau vijana 15,000.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku07 February 2024 - 10:39

Muhtasari


• Mamlaka haikutoa sababu mara moja ya hatua hiyo lakini waliahidi kutoa taarifa mwishoni mwa zoezi hilo, vyombo vya habari vya ndani viliripoti.

Baadhi ya vijana hao walihoji uamuzi wa kuwafungia nje ya zoezi hilo kwa sababu tu ya sanaa yao ya mwili

Vijana kadhaa wa Kenya wamefungiwa nje ya usajili unaoendelea katika shirika la vijana la serikali kwa kuchora tattoo kwenye miili yao.

Ingawa walitimiza sifa za kitaaluma na pia kufaulu mtihani wa utimamu wa mwili ili kujiunga na Huduma ya Kitaifa ya Vijana (NYS), walionekana kutostahiki kwa sababu ya kuchora tattoo.

Baadhi ya vijana walioondolewa walihoji uamuzi wa kuwafungia nje ya zoezi hilo kwa sababu tu ya usanii wao na kuzitaka mamlaka hizo kuangalia upya hatua hiyo.

Mamlaka haikutoa sababu mara moja ya hatua hiyo lakini waliahidi kutoa taarifa mwishoni mwa zoezi hilo, vyombo vya habari vya ndani viliripoti.

Shughuli ya uajiri wa NYS, ambayo inafanyika kote nchini, ilianza Jumatatu, na inatafuta kuajiri angalau vijana 15,000.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved