logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kaka Mkubwa wa Jose Chameleone amefariki baada ya kuugua saratani

Ugonjwa wa Humphrey Mayanja uligunduliwa Julai mwaka jana, alipowasili Marekani akitokea Uganda.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku30 March 2024 - 07:51

Muhtasari


• Chameleone aliweka picha ya Humphrey kwenye ukurasa wake wa Facebook ikiwa na jina lake tu na emoji ya kilio.

Kakake Chameleone amefariki

Mwanamuziki Humphrey Mayanja, kaka wa gwiji Jose Chameleone amefariki dunia.

Humphrey alishindwa katika vita dhidi ya saratani katika Taasisi ya Saratani yenye makao yake Mulago nchini Uganda.

Chameleone aliweka picha ya Humphrey kwenye ukurasa wake wa Facebook ikiwa na jina lake tu na emoji ya kilio.

Familia yake ilikuwa imemrudisha hivi karibuni kutoka Marekani ili kupata matibabu karibu na nyumbani na kuzungukwa na watu wake.

Ugonjwa wa Humphrey Mayanja uligunduliwa Julai mwaka jana, alipowasili Marekani akitokea Uganda.

Alikimbizwa hospitalini akiwa na maumivu makali ya tumbo na kufanyiwa upasuaji mkubwa.

Mapema mwezi huu, babake Gerald Mayanja alithibitisha kuwa mtoto wake mkubwa wa kiume alikuwa akitibiwa saratani ya utumbo mpana hatua ya nne.

Alisema waliamua kumrudisha Uganda ili kupata matibabu karibu na ho


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved