logo

NOW ON AIR

Listen in Live

IPOA yaanza uchunguzi baada ya mwanamume,19,kupigwa risasi Kirinyaga

IPOA katika taarifa ya Jumatatu, Mei 20, 2024, ilisema imeanza uchunguzi

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku20 May 2024 - 12:12

Muhtasari


  • Wenyeji walifanya vurugu kufuatia ufyatulianaji risasi huo, wakitaka mamlaka ya eneo hilo ipewe maelezo baada ya afisa wa polisi kuhusishwa na tukio hilo.
Mwanafunzi ajiua kwa kujipiga risasi Kilimanjaro

Mamlaka Huru ya Uangalizi wa Polisi (IPOA) imeanza uchunguzi kuhusu mauaji ya kijana wa miaka 19 katika kituo cha kibiashara cha Kiandai Gichugu, Kaunti ya Kirinyaga.

IPOA katika taarifa ya Jumatatu, Mei 20, 2024, ilisema imeanza uchunguzi kama ilivyoamrishwa chini ya Sura ya 86 ya katiba ya Kenya.

"IPOA, kama ilivyoamrishwa chini ya Sura ya 86 ya sheria za Kenya, imeanza uchunguzi kuhusu mauaji ya kijana katika Kaunti ya Kirinyaga siku ya Jumapili," mamlaka hiyo ilisema.

Wenyeji walifanya vurugu kufuatia ufyatulianaji risasi huo, wakitaka mamlaka ya eneo hilo ipewe maelezo baada ya afisa wa polisi kuhusishwa na tukio hilo.

Derrick Gachoki aliuawa kwa kupigwa risasi saa kumi na mbili jioni wakati maafisa wa polisi waliokuwa wakishika doria walipofika katika kituo cha soko.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved