logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pasta Ng'ang'a amkashifu Kanyari kufuatia matendo yake mitandaoni

Ng'ang'a alimkosoa Kanyari kwa tabia yake ya kutatanisha mtandaoni iliyosababisha hasira ya umma.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku27 May 2024 - 08:23

Muhtasari


•Mchungaji James Ng'ang'a alimkosoa waziwazi nabii Victor Kanyari kwa tabia yake ya kutatanisha mtandaoni iliyosababisha hasira ya umma.

•Mchungaji Ng'ang'a alitilia shaka kukosekana kwa maendeleo katika huduma ya Kanyari, akibainisha kuwa bado hana kanisa licha ya miaka ambayo imepita.

Mhubiri James Ng'ang'a amemkashifu nabii Victor Kanyari kufuatia matukio yake ya hivi majuzi kwenye mtandao wa tiktok  ambayo yalizua utata na kuibua gumzo miongoni mwa umma.

Akizungumza wakati wa mahubiri katika kanisa lake la Neno Evangelism Centre, Ng'ang'a alitoa matamshi yake yaliyoonekana kumlenga mhubiri huyo mwenzake.  

Mhubiri huyo alisema aliacha  kutumiaTikTok kwa sababu ya watu wasio na adabu ambao wanatumia mtandao huo.  

"Niliondoka TikTok baada ya kuona takataka kutoka kwa viumbe hawa. Kwa nini wahubiri hawa hawakufi?"

Alisema kuwa anaomba sana Mungu alete mafuriko pamoja na radi ili kuwaadhibu watu ambao wanafanya makosa kwa kizazi hiki.

“Natamani sana Mungu alete radi itupige sisi wote pia mimi kama niko miongoni mwao kwa sababu jinsi watu wanavyoenda kiholela na kumkosea Mungu na hiki kizazi kibaya” aliongezea.

Aliendelea kubainisha jinsi alivyohubiri katika kanisa hiyo ya Kanyari na kudai bado hajabadilika na hakuna maendeleo amefanya tangu wakati huo.

 "Nilihubiri katika eneo lake nilipofika Nairobi, yeye alikuwa Kawangware, na mpaka sasa, bado yuko huko bila kanisa ikiwa haujamaliza mambo ya kidunia, kaa huko, usichanganye haya mambo mawili Miaka yote hii na hana hata kanisa, lile la Kamulu, eneo la Mkuru. Nilimuacha pale na bado yuko palepale.” Mchungaji Ng’ang’a pia alisema.

Alisema afadhali yeye aende mbinguni uchi na bila utajiri wowote lakini akuwe na wokovu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved