logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Cleo Malalah aunga mkono ajenda ya vuguvugu la Tawe

Malalah ameunga mkono ajenda ya Tawe movement huku akiwataka Oparanya na Eugene kujiuzulu kwa siasa.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku03 June 2024 - 09:09

Muhtasari


•Cleophas Malala ameunga mkono ajenda ya Tawe Movement inayoongozwa na Gavana George Natembeya wa Trans Nzoia.

•Natembeya aliwashutumu Mudavadi na Wetang'ula kwa kukosa kuleta maendeleo ya Magharibi licha ya kuwa serikalini kwa miongo kadhaa.

Katibu mkuu wa UDA Cleophas Malala

Katibu Mkuu wa Chama cha United Democratic Alliance (UDA) Cleophas Malala ameunga mkono vuguvugu la Tawe la gavana wa Trans Nzoia George Natembeya.

Akizungumza katika kaunti ya Vihiga, Malala alisema anaunga mkono kikamilifu ajenda inayoongozwa na Natembeya, inayotaka katibu mkuu wa baraza la mawaziri Musalia Mudavadi na spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang'ula kustaafu kutoka kwa siasa.

Malala alimtaka Natembeya kuwaongeza aliyekuwa gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya na aliyekuwa waziri wa ulinzi Eugene Wamalwa kwenye ajenda za vuguvugu hilo.

"Naunga mkono kikamilifu ajenda yako huko Trans Nzoia; nimeona ukiwasukuma Wetang'ula na Mudavadi waende nyumbani. Hata hivyo, orodha haijajaa; hata Oparanya na Eugene wanafaa kwenda nyumbani kupumzika," Malala alisema.

Aidha Malala pia alikashifu mpango wa Oparanya kuwania useneta wa Kakamega 2027. Malala alisema ni wakati wake wa kupumzika kutoka kwa siasa, kwani amekuwa mamlakani tangu enzi za Ford Asili.

Baadhi ya wanasisa kama  vile mbunge wa UDA Gathoni Wamuchomba pia  wameunga mkono ajenda ya Gavana Natembeya. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved