logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kutana na mrembo ameishi na ubikira kwa miaka 33 kwa kuwa na masharti 12 kwa wanaume

"Nina viwango vya juu na sidanganyi," alisema katika mahojiano, iliyoripotiwa na New York Post.

image
na Davis Ojiambo

Burudani21 June 2024 - 12:57

Muhtasari


  • • Noble yuko sana kwenye mitandao ya kijamii, ambapo anashiriki shughuli zake za kila siku. Ingawa anataka uhusiano, anachagua sana.
  • • "Nina viwango vya juu na sidanganyi," alisema katika mahojiano, iliyoripotiwa na New York Post.
  •  
    • Noble alikiri kuwa hajawahi kuwa kwenye uhusiano mzito. Uhusiano wake mrefu zaidi ulidumu siku tatu tu. Licha ya hayo, yeye haachi tumaini la kupata mwenzi kamili.
DONYELLE NOBLE

Mrembo mmoja mwenye umri wa miaka 33 amedai kuwa masharti yake magumu kwa wanaume wanaojaribu kumtongoza yamesababisha yeye kuwa bikira hadi sasa.

Kwa mujibu wa jarida la The New York Post, Danyele Noble kutoka jimbo la Florida anaorodhesha vigezo 12 ambavyo mwanaume lazima afikie kabla ya kuamua kuwa na uhusiano naye.

Kutokana na hilo, wanaume wengi ambao wanashindwa ku’tick maboksi yote 12 wameishia kumtenga na mpaka kufikia umri wa miaka 33, bado hajawai kushiriki tendo la ndoa ila anatumai mwanamume wake yupo njiani.

Noble yuko sana kwenye mitandao ya kijamii, ambapo anashiriki shughuli zake za kila siku. Ingawa anataka uhusiano, anachagua sana.

"Nina viwango vya juu na sidanganyi," alisema katika mahojiano, iliyoripotiwa na New York Post.

Noble alikiri kuwa hajawahi kuwa kwenye uhusiano mzito. Uhusiano wake mrefu zaidi ulidumu siku tatu tu. Licha ya hayo, yeye haachi tumaini la kupata mwenzi kamili.

"Nilikuwa nikiona aibu kuwaambia watu kuhusu hilo. Ningependa kusema uwongo tu na kusema, 'Hapana, mimi si bikira,' lakini kuzungumza juu yake mara kwa mara kumenifanya nitambue kwamba hakuna ubaya na hilo. Watu wengi wanaheshimu hilo."

Mahitaji yake yanahusu sifa zote mbili za utu na mwonekano wa mwenzi anayewezekana.

Kwa mujibu wa jarida hilo, Noble anaangazia mwanamume kuwa; mkweli, Mwenye moyo mwema, Mrefu kuliko yeye, mwenye mwili wa kiriadha-riadha hivi, anayependa kusafiri, anayependa maisha ya nje ya nyumba, mwenye hajawahi kuoa awali, mwenye uthubutu, mcheshi, mtulivu, na wa kumheshimu yeye.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved