logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamke adai yeye ndiye ‘Bikira Maria Mtakatifu’ mama wa Yesu (video)

Alishikilia kuwa yeye ni mama yake Yesu na Maria Mtakatifu kwenye video hiyo.

image
na Davis Ojiambo

Burudani21 June 2024 - 13:58

Muhtasari


  • • Katika video hiyo, mwanamke huyo anasikika akizungumza kuhusu kuwa na maono wakati akitangaza kuja kwa Yesu duniani.
Anayedai kuwa Maria mama wa Yesu

Mwanamke mmoja kutoka nchini Nigeria anayedai kuwa yeye ni Mariamu mtakatifu amezua mjadala akidai Yesu anatoka Nigeria.

Hii ilifichuliwa katika chapisho jipya lililozua mawimbi kwenye jukwaa maarufu la mitandao ya kijamii.

Katika video hiyo, mwanamke huyo anasikika akizungumza kuhusu kuwa na maono wakati akitangaza kuja kwa Yesu duniani.

 

Anasikika akifichua kuwa yeye ni Bikira Maria kama ilivyofunuliwa kwake, huku akitangaza kwa ujasiri kwamba Yesu ni Mnigeria kutoka Jimbo la Imo, haswa kutoka eneo la serikali ya mtaa liitwalo Mbaitoli.

 

Alishikilia kuwa yeye ni mama yake Yesu na Maria Mtakatifu kwenye video hiyo, ambayo imevutia maelfu ya watu waliotazamwa mtandaoni.

Kwa maneno yake;

“Ndio, Yesu anatokea Nigeria. Mimi ndiye mama wa Yesu na yeye usuli wake ni Nigeria. Mungu alinifunulia kujua kwamba mimi ndiye mama wa Yesu. Na huu ufunuo umekuwa ukinijia tangu 2015, nimekuwa nikipata maono mengi na Yesu alizaliwa kupitia mimi.”

“Kwa mujibu wa maono ambayo ninapata, mimi ndiye Bikira Maria mtakatifu mama wa Yesu na Yesu atakuja tena kupitia mimi katika ujio wake wa pili duniani, na hicho ndicho ambacho Mungu ameniagiza kutangaza.”

Tazama video hiyo hapa chini kisha utoe maoni yako.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved