logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Malezi kisasa! Zari na wanawe waonekana wakiburudika pamoja, kubugia mvinyo na kuvuta shisha (+picha)

Mwanawe Zari, Pinto Tale alisherehekea siku yake ya kuzaliwa mnamo Jumatatu, Agosti 8.

image
na SAMUEL MAINA

Burudani08 August 2023 - 09:46

Muhtasari


  • •Zari alionyesha klipu za video na picha zake na wanawe katika kilabu cha kifahari ambapo walionekana kuwa na wakati mzuri.
  • •Huku akimtakia heri ya siku ya kuzaliwa mwanawe Pinto Tale , Zari Hassan alimhakikishia upendo wake mkubwa kwake.
pamoja na wanawe Pinto Tale na Raphael Ssemwanga.

Siku ya Jumatatu, mwanasholaiti na mfanyabiashara maarufu wa Uganda  Zari Hassan alionekana akiburudika katika kilabu pamoja na wanawe wawili wakubwa Pinto Tale na Raphael Ssemwanga Jr

Katika ukurasa wake wa Instagram, mama huyo wa watoto watano alionyesha klipu za video na picha zake na wanawe katika kilabu cha kifahari ambapo walionekana kuwa na wakati mzuri.

Katika video hizo, watatu hao ambao pia walikuwa pamoja na marafiki wengine wa wanawe Zari walionekana kuwa na furaha nyingi na tabasamu kwenye nyuso zao zilidhihirisha hilo

Katika video moja,  Zari alionekana akibugia glasi ya mvinyo huku mwanawe mkubwa, Pinto Tale akirekodi matukio hayo ya kufurahisha kwa kutumia kamera ya simu. Video nyingine ilimuonyesha Raphael akivuta moshi wa shisha huku mama yake akiwa amemshika kwenye bega.

Haikuwa mara ya kwanza kwa Zari kuonekana na wanawe klabuni hapo, katika siku za nyuma aliwahi kuandamana nao kwenda kujiburudisha kwenye vilabu mbalimbali na kisha kurekodi matukio hayo kwenye mitandao ya kijamii.

Mwanawe Zari, Pinto Tale alisherehekea siku yake ya kuzaliwa mnamo Jumatatu, Agosti 8.

Huku akimtakia mwanawe heri ya siku ya kuzaliwa, mpenzi huyo wa zamani wa staa wa bongo Diamond Platnumz alimhakikishia upendo wake mkubwa kwake.

"Heri ya kuzaliwa Pinto Tale. Kijana, inaonekana wewe si shabiki wa shots moja. Nakupenda kido,” Zari alimwandikia mwanawe, Pinto Tale kwenye Instagram.

Ni mara nyingi ambapo mfanyibiashara huyo anayeishi Afrika Kusini ameonekana akijumuika na Pinto Semwanga ,20,  na Raphael  Semwanga ,17, kujivinjari pamoja na marafiki zao kwenye maeneo mbalimbali ya burudani. 

Hii ni moja tu ya viashirio vingi vinavyoonyesha kuwa mwanasoshalaiti huyo ana uhusiano wa karibu sana na watoto wake.

Kujivinjari pamoja na wanawe bila kuzingatia pengo kubwa kati ta umri wake na wao sio jambo la kawaida hasa barani Afrika.

Kando na hilo, Zari ameonekana kuwa tofauti sana na wazazi wengi wa Kiafrika kuhusu jinsi ya kusimamia mali na biashara za familia.

Mfanyibiashara huyo mwenye umri wa miaka 42 amewaaminia  kwa kiwango kikubwa wanawe wakubwa  na usimamizi wa biashara  na mali  nyingi iliyoachwa nyuma na aliyekuwa mumewe marehemu Ivan Semwanga.

Mapema mwaka jana, Zari alianzisha mchakato wa kuhamisha uongozi wa Chuo cha Brooklyn City kwa watoto wake.

Mnamo mwezi Januari 2022, mzaliwa huyo wa Uganda alitumia ukurasa wake wa Instagram kutangaza kuwa amemteua mwanawe mkubwa Pinto Ntale kuwa Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Chuo hicho.

"Mkurugenzi Mtendaji Mkuu. mafunzo, wafundishe wangali vijana, siwezi kusubiri kumwona akichukua kampuni na kusimamia fedha,” Zari alisema.

Lingine linalomtofautisha Zari na wazazi wengine ni jinsi anaendeleza ushirikiano mzuri katika malezi na mzazi mwenzake Diamond Platnumz.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved