Muhtasari
• Mwanablogu, Presenter Ali amemkashifu vikali msanii Magix Enga kwa kile anachokitaja kuwa ni kutumia jukwaa lake kutoa stori za uongo ili kufufua kipaji chake ambacho kilikuwa kimeonekana kufifia.
• Presenter Ali ambaye ameonekana kuwa mwenye gadhabu katika video moja aliyoiachia katika mtandao wa YouTube akisema kwamba, msanii huyo ambaye pia ni mzalishaji wa muziki amemkosea heshima na kusisitiza kuwa hakuhusika kivyovyote vile katika njama hizo za Magix Enga kuwahadaa mashabiki.
• Presenter Ali amewaomba msamaha mashabiki wake na kuahidi kuzidi kuwapa kazi za kuburudisha.