Bila huyu mzungu mimi ningekuwa nimezikwa-Akothee amsifia baby daddy wake

Akothee alieleza jinsi baby daddy wake alimwinua kutoka chini na kumfanya awe malkia na maisha ambayo anaishi sasa.

Muhtasari
  • Msanii huyo ameenda kuwatembelea wanawe, na huku akimsifia baby daddy wake amesema kwamba bila yeye hangekuwa hai leo
Image: HISANI

Wengi wanamfahamu kutokana na bidii ya kazi yake, na jina lake ambali hujiita 'presie\dent of single mothers'.

Akothee ni miongoni mwa watu mashuhuri ambao wanaishi maisha ya kifahari humu nchini.

Msanii huyo ameenda kuwatembelea wanawe, na huku akimsifia baby daddy wake amesema kwamba bila yeye hangekuwa hai leo.

Akothee alieleza jinsi baby daddy wake alimwinua kutoka chini na kumfanya awe malkia na maisha ambayo anaishi sasa.

Pia msanii huyo aliwarushia makombora wakosoaji wake na kuwashauri wanapaswa kutafuta mzungu pia abadilishe maisha yao.

"Bila huyu mzungu mimi ningekuwa nimezikwa.Mimi aliniokolea ,mimi sijui unaokolewa na nani ,na ninajua wako kama wanaume 20 ,ni vile hatukujui ,so usitupimie hewa. Wewe unaitisha beer ,nyama choma na simu ,sister, tunaitisha shamba na biashara .

Mchezo ni mmoja na wachezaji tofauti, na kiwango tofauti. miliki kiwango chako.chukia mchezo wenyewe na wala sio mchezaji 🤣🤣🤣🤣🤣😍🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Wengine wanaongea na wamewekwa na kuzaa na mabwana za watu 🤣🤣I AM LIVING THE LIFE YOU WISH ,OTHERWISE I WOULD BE COMMENTING SHIT ON YOUR WALL TOO IF YOU HAD THIS LIFE THAT INAM LIVING 🤣🤣🤣🤣."