β’ Ni kama mimi siwezi chumbiana na mtu anasikiliza Reggae - Vera Sidika.
Mwanasosholaiti mstaafu Vera Sidika amedokeza kwamba yeye pia hawezi kujipata au hata kuwaza tu kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na mtu ambaye anasikiliza miziki aina ya Reggae.
Mama huyo wa mtoto mmoja alikuwa akiyasema haya baada ya mtangazaji maarufu Kanene Goro kuweka wazi kwamba yeye ni vigumu kuchumbiana na mwanaume mwenye miziki yake ni ya Reggae.
Vera Sidika alipakia picha ya habari hizo na kusema kwamba mtangazaji huyo hayupo peke yake kwani wapo wanawake wengi nyuma yake ambao hawana mapenzi hata kidogo na watu wanaosikiliza miziki ya mitindo taratibu ya Reggae.
βHuyu ni kama mimi kabisaaa,β Vera Sidika alipakia kwenye instastories zake alizungumzia matamshi ya mtangazaji huyo.
Vera Sidika ni mamake mtoto Tajiri Asia Brown na ameolewa na mwanamuziki wa ngoma za kizazi kipya Brown Mauzo.
Baada ya Vera Sidika kutolea maoni hayo kumuunga mkono mtangazaji huyo, watu mbali mbali walishindwa kujizuia na walikuwa na maoni kinzani.
Wengine walimsuta kwa kuzungumzia mambo ya kuchumbiana na tayari yuko kwenye ndoa na msanii Mauzo pamoja na kuwa na mtoto juu huku wengine wakimtania kwamba watu wa rasta hata wao hawapendi kabisa kuchumbiana na wanadada mikorogo wa kujichubua.
βVera Sidika ako kwa ndoa na anaongea stori za kudateπππdunia ni ngumu,β shabiki kwa jina Muriithi Caleb aliandika.