Mapenzi na Kazi: Wachumba ambao pia ni washirika kikazi

Hawa ni wale waliokiuka dhana ya kuwa mapnezi kazini hayawezi yakapaliliwa na kua.

Muhtasari

• Hapa tunakuandalia orodha ya baadhi ya Wakenya maarufu ambao wamefanikiwa pakubwa kukiuka dhana hizo zinazoonya dhidi ya kuwa na mpenzi ambaye mnafanya kazi pamoja.

Wachumba wanaofanya kazi pamoja
Wachumba wanaofanya kazi pamoja
Image: Instagram

Kuna dhana nyingi tu zinazohusisha mapenzi na kazi, wengi huonya dhidi ya kujiingiza mapenzi na mtu ambaye mnafanya kazi pamoja, lakini je, unafahamu wapo baadhi ya Wakenya maarufu ambao ni wachumba au wapenzi na wanafanya kazi kwa pamoja?

Hapa tunakuandalia orodha ya baadhi ya Wakenya maarufu ambao wamefanikiwa pakubwa kukiuka dhana hizo zinazoonya dhidi ya kuwa na mpenzi ambaye mnafanya kazi pamoja.

Wahu na Nameless

Hao ni wapenzi wa zaidi ya miaka 25 ambao wanasherehekewa sana kuwa watu maarufu waliokiuka dhana zote zinazolenga kutoa tafsiri kuwa mapenzi na kanzi haviwezi vikaendana. Katika safari yao ya pamoja kama wapenzi kwa miaka 25 iliyopita, Wahu na Nameless wanajivunia ndoa imara na mabinti watatu juu.

Wamekuwa wakishirikiana katika kazi za kimuziki miaka hiyo yote na mwaka jana waliachia collabo yao ya Back It Up ambayo mpaka sasa inazidi kufanya vizuri katika masoko mbalimbali ya kidijitali ya kupakua miziki.

Lulu Hassan na Rashid Abdalla

Image: INSTAGRAM// LOULOU HASSAN

Watangazaji mashuhuri wa habari ambao hutumika kama mfano bora kwa wengi kwenye mitandao ya kijamii. Lulu na Rashid wanafanya kazi pamoja kwenye Citizen TV kama waandaaji wenza wa taarifa ya habari ya Nipashe ya Citizen.

Diana Marua na Bahati Kioko

Bahati na mkewe Diana Marua
Image: INSTAGRAM// DIANA MARUA

Wapenzi hawa wawili ambao wiki hii walimpokea mtoto wao Malaika wamekuwa wakifanya kazi pamoja kwa muda mrefu tangu msanii Bahati aache kuwasajili wasanii wapya kwenye lebo ya EMB.

Pamoja kama wachumba, wamekuwa wakishirikiana katika miradi mbali mbali ya nyimbo huku wakitoa collabo zilizoteka anga na kupendwa na wengi.

Milly na Kabby wa Jesus

Image: INSTAGRAM// KABI WAJESUS

Hii ni familia ya wanablogu wa mtandao wa YouTube ambao wamefanikiwa kufanya kazi pamoja na kupata ufanisi usiomithilika kutokana na ushirikiano wao wa kuunda maudhui ya YouTube.

Wameonyesha mtindo wa maisha unaoongozwa na kudumishwa na mikataba ya ubalozi wanayopata kutoka kwa makampuni mbali mbali kutokana na ufuasi mkubwa walionao kwenye chaneli yao ya pamoja ya YouTube.

Milly Chebby na Terence Creative

Terence Creative na mkewe Milly Chebby
Terence Creative na mkewe Milly Chebby
Image: Terence Creative//Facebook

Milly Chebby na Terrence Creative hutengeneza video pamoja, wakionyesha taratibu zao za maisha ya kila siku na mambo mengine yanayozunguka maisha ya kila siku ambayo huburudisha wafuasi wao. Hukuwakiwa wamedumu pamoja kwa zaidi ya miaka 10, wawili hawa wamefanikiwa pakubwa kutokana na mitikasi yao ya mitandaoni.

Mungai Eve na Trevor

instagram KWA HISANI
instagram KWA HISANI
Image: mungai eve

Moja kati ya wanandoa mashuhuri wachanga zaidi nchini Kenya. Mungai Eve na mpenzi wake ambaye pia anajiongeza kama muongozaji wa video zao walianza kutoka chini hadi sasa wanatamba katika tasnia ya burudani kwani wana chaneli ya YouTube inayokua kwa kasi pamoja ambayo ni biashara yao yenye malipo kama wanandoa.

Celestine na Njugush

Njugush na Celestine wamefanikiwa sana kwenye YouTube wakitengeneza skits za kuchekesha ambazo zimewafanya waendelee kuunda maudhui zaidi pamoja kwenye mitandao ya kijamii.

Image: INSTAGRAM// CELESTINE NDINDA

Pamoja wamefanikiwa kununua nyumba nzuri na wana watoto wawili, mwa pili wakitangaza kumkaribisha hivi majuzi. Wamekuwa wakifanya mwendelezo wa filamu yao ya Through Thick &Thin ambayo inasimulia jinsi waligandiana tangu wakiwa bila kitu mpaka sasa wakiwa angalau na utajiri wa kusitiri maisha yao ya kila siku.

Kate Actress na Phillip Karanja

Phil na Kate Actress walipata upendo kwa kila mmoja wakati wakifanya kazi pamoja. Kate, ambaye jina lake halisi ni Catherine Kamau, aliwahi kusimulia hadithi ya jinsi yeye na mumewe walipatana. Alisema awali hawakuweza kusimama kila mmoja kwenye seti. Hivi sasa, wanandoa wana kampuni yao ya uzalishaji kwa jina la Phil It Productions.

 

 

Judy Nyawira na Abel Mutua

katika hafla ya awali.
Muigizaji Abel Mutua na mke wake Judy Nyawira katika hafla ya awali.
Image: INSTAGRAM// JUDY NYAWIRA

Abel Mutua amekuwa akimtumia mkewe Judy Nyawira kama mtayarishaji/meneja wake. Judy hupanga matoleo mengi ya Abel kwenye YouTube, kazi ambayo mashabiki wao wengi wamewasifia.

Nadia Mukami na Arrow Bwoy

Image: INSTAGRAM// NADIA MUKAMI

Wawili hao ambao miezi michache iliyopita walimkaribisha mtoto wao wa kwanza wamekuwa wakifanya muziki pamoja kabla na hata baada ya kupendana.

Nadia Mukami na Arrow Bwoy walishirikiana katika nyimbo kadhaa na wimbo wao wa hivi majuzi, 'Kai Wangu' uliochochewa na mtoto wao wa kiume.

Jackie Matubia na Blessing Lungaho

Image: INSTAGRAM// JACKIE MATUBIA

Kuna habari kwamba waigizaji hao mahiri walikutana kwenye seti ya kipindi cha Zora wakati Jackie Matubia akicheza 'Nana' na Blessings akacheza 'Madiba'.

Wawili hao walioigiza 'struggle love' hivi majuzi walimkaribisha mtoto wao wa kwanza pamoja na pia wamechumbiana.