Bahati atangaza mapenzi yasiyoisha kwa bintiye wa kwanza Mueni

Bahati pia alifichua mapenzi yake yasiyoisha kwa bintiye. Aliapa kwamba atakuwa tayari kumsaidia Mueni kila wakati.

Muhtasari
  • Bahati ni baba  wa watoto watatu na Diana. Mtoto mdogo zaidi, Malaika, alizaliwa siku chache zilizopita
Image: INSTAGRAM// DIANA MARUA

Mwanamuziki maarufu Bahati ametangaza kwamba atakuwepo kila wakati kwa binti yake wa kwanza Mueni.

Bahati pia alifichua mapenzi yake yasiyoisha kwa bintiye. Aliapa kwamba atakuwa tayari kumsaidia Mueni kila wakati.

Mueni ni binti ya Bahati na mpenzi wake wa zamani, Yvette. Walibarikiwa na mtoto lakini walitengana baada ya muda mfupi.

Mwimbaji huyo aliendelea na  kuoa mke wake wa sasa, Diana.

Bahati ni baba  wa watoto watatu na Diana. Mtoto mdogo zaidi, Malaika, alizaliwa siku chache zilizopita.

Wanandoa hao walifurahi kumkaribisha mtoto wao baada ya safari ya ujauzito yenye changamoto

Mueni alionekana kufurahi sana kuwa pamoja na baba yake, Bahati.

Walishikana mikono na kutabasamu kipindi hicho. Hii ilionyesha wazi kwamba wanafurahia mapenzi ya baba na binti Hakika wanapendana.

"Kwa Binti Yangu mzaliwa wa kwanza. Nitakuwa hapa kwa ajili yako kila wakati. Daima nitakuwa Shabiki wako Mkuu. Nakupenda kwa moyo wangu wote ❤,"Bahati Aliandika.