Unataka kuwaadhibu makamishna wa IEBC-Ledama amkashifu Ruto

Makamishna hao walijitenga na matokeo yaliyompa Ruto ushindi dhidi ya kiongozi wa Azimio One Kenya Raila Odinga.

Muhtasari
  • Ledama alisema huku Ruto akiwa amevuka changamoto iliyotishia urais wake, anafaa kuacha mapigano hayo
Ole Kina asema Ruto aliwahadaa wananchi
Ole Kina asema Ruto aliwahadaa wananchi
Image: Facebook

Seneta wa Narok Ledama Olekina amemkashifu Rais William Ruto kuhusu hatua ya kuwaondoa makamishna wanne wanaopinga IEBC.

Katika taarifa yake siku ya Alhamisi, mwanasiasa huyo alisema mchakato wa kuwatimua makamishna hao haukuwa na dhamira kwa vile Ruto sasa ni Rais.

"Je, si jambo la kushangaza kwamba sasa unataka kuwaadhibu makamishna wa IEBC ilhali umepata ushindi? Acha vita hivi visivyo vya lazima. Si thamani yake."

Wanne hao walitofautiana na mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati wakati wa uchaguzi wa urais wa Agosti, na kufichua kutoelewana katika shirika la uchaguzi.

Makamishna hao walikashifu matokeo yaliyompa Ruto ushindi dhidi ya kiongozi wa Azimio One Kenya Raila Odinga.

Ledama alisema huku Ruto akiwa amevuka changamoto iliyotishia urais wake, anafaa kuacha mapigano hayo.

“Mheshimiwa Rais, nilifikiri ulisema tofauti ya walioshinda na walioshindwa katika uchaguzi uliopita ni wale waliomwamini Mungu dhidi ya Wanadamu?,” alisisitiza.

Taarifa yake inajiri saa chache baada ya viongozi wa muungano wa Azimio kuapa kusimama na makamishna hao wa IEBC.