Wenye hisa waishtaki Adidas kwa kuvunja mkataba na Kanye West kupelekea hasara kubwa

Oktoba mwaka jana, Adidas ilikatisha mkataba na Kanye kufuatia matamshi yake ya uchochezi dhidi ya Wayahudi.

Muhtasari

• Adidas waliathirika pakubwa kufuatia kukatishwa kwa mkataba na Yeezy ya Kanye huku pia msanii huyo akiathirika kwa kuporomoka kutoka hadhi ya ubilionea.

• Adidas ilifichua kuwa kusitishwa kwa mkusanyiko wa mitindo kutagharimu chapa hiyo dola bilioni 1.3 kwa mauzo mwaka huu.

Adidas yaonya kupoteza faida baada ya kuachana na Kanye West
Adidas yaonya kupoteza faida baada ya kuachana na Kanye West
Image: BBC NEWS

Wanahisa wa kampuni ya Adidas wamefungua kesi dhidi ya kampuni hiyo kubwa ya nguo za michezo kutokana na kukatishwa kwa ushirikiano wa kampuni hiyo na rapa maarufu Kanye West.

Katika kesi hiyo iliyowasilishwa Ijumaa katika Mahakama ya Wilaya ya Portland ya Marekani, wanahisa hao walidai kuwa watendaji wa kampuni hiyo walikuwa wanafahamu hatari zinazoletwa na tabia ya West miaka kadhaa kabla ya mzozo huo, lakini hawakuchukua hatua za tahadhari, ripoti za habari za NBC zinaripoti.

"Katika sehemu ya Hatari ya Wafanyikazi katika mjadala wa Ripoti ya 2018 ya hatari, Kampuni ilisifu dhamira yake ya kuwa na sehemu ya kazi yenye usawa, na mchakato wake wa kimkakati wa usimamizi wa wafanyikazi, unaojulikana kama 'Mkakati wa Watu', huku ikishindwa kujadili jinsi ilivyopuuza mara kwa mara tabia mbaya kutoka kwa Kanye West,” ilisomeka kwa sehemu.

Wakirejelea ripoti ya Wall Street Journal ya Novemba 2022, walalamikaji walisema zaidi kwamba afisa mkuu mtendaji wa zamani wa Adidas, Kasper Rorsted, na afisa mkuu wa fedha, Harm Ohlmeyer, "walikusudia kuwahadaa" wawekezaji au "walifanya bila kujali ukweli" kwa kuwaweka wanahisa gizani kuhusu masuala kati ya kampuni na rapper huyo.

Ikinukuu watu wanaofahamu suala hilo, ripoti ya WSJ ilifichua kwamba mtendaji mkuu wa kampuni hiyo na maofisa wakuu nchini Ujerumani walijadili tangu mwaka wa 2018, hatari za kudumisha uhusiano na rapper huyo wa 'Monster', ambao walihofia unaweza kulipuka wakati wowote.

Huko nyuma mnamo 2018, West pia alikuwa ametoa taarifa za uchochezi kuhusu utumwa. Wakati wa mahojiano na TMZ, rapper huyo alisema kuwa miaka 400 ya utumwa iliyoteswa na watu weusi huko Amerika "inasikika kama chaguo".

Wanahisa zaidi waliwalaumu watendaji kwa kutotaja mahususi katika ripoti za kila mwaka “kwamba Kampuni ilikuwa imefikiria kukomesha ushirikiano kutokana na tabia ya kibinafsi ya West, au jinsi sifa ya Kampuni inaweza kuathiriwa ikiwa tabia yake, kama ilivyohusiana na Kampuni, ingeathiriwa kama ingewekwa hadharani.”

Kampuni hiyo ya Ujerumani hatimaye ilikata uhusiano na Ye mnamo Oktoba mwaka jana kufuatia mfululizo wa kauli za chuki dhidi ya Wayahudi alizotoa kupitia majukwaa mbalimbali ya vyombo vya habari mwaka jana. Kampuni hiyo ilikabiliwa na shinikizo kubwa kutoka kwa umma baada ya msanii huyo kusisitiza maradufu matamshi yake licha ya chuki za awali na kupigwa marufuku kutoka kwa mitandao ya kijamii.

 

Ushirikiano uliofeli wa Yeezy uligharimu pande zote mbili, kwani West alipoteza hadhi yake ya bilionea mwaka jana. Mnamo Februari, Adidas pia ilifichua kuwa kusitishwa kwa mkusanyiko wa mitindo kutagharimu chapa hiyo dola bilioni 1.3 kwa mauzo mwaka huu.