Mamake mtoto anayedai kuwa wa Jay-Z adai kondomu ‘ilipasuka’ wakati wa kujamiiana

"Sikumwona tena hadi miaka kadhaa baadaye kwenye runinga lakini bado sikujua jina lake halisi hadi baadaye na sikujua jinsi ya kumfikia," hati ya kiapo ilisoma.

Muhtasari

• Walakini, chanzo kiliambia Page Six kwamba Jay-Z "hajawahi kukutana na mwanamke huyo."

Mwanamume ajitokeza akidai DNA na Jay-Z
Mwanamume ajitokeza akidai DNA na Jay-Z
Image: Mail Online//screengrab

Wiki jana,Radio Jambo tuliripoti kuhusu kesi ambayo mwanamume wa miaka 30 aliwasilisha mahakamani akidai vipimo vya sampuli za DNA za msanii Jay-Z kwa kile alisema kuwa mamake alimwambia ndiye babake kipindi ako na miaka minane.

Sasa jarida la Page Six limezama Zaidi na kuibuka na ripoti mpya kwamba mama wa jamaa huyo aliwahi kuandika kwa kina kuhusu jinsi alivyopata ujauzito wa mwana wa Jay-Z mwaka wa 1992.

Walakini, chanzo kiliambia Page Six kwamba Jay-Z "hajawahi kukutana na mwanamke huyo."

“Hamjui. Hii si kweli, "chanzo kinachofahamu hali hiyo kinatuambia, kikibaini kwamba hati ya kiapo iliyopatikana na Daily Mail Friday inaweza hata isiwe "halisi" kwani "haijawasilishwa mahakamani."

"Jay-Z hata hamjui mtu huyu."

Kulingana na jarida hilo, mwanamke huyo, Wanda Satterthwaite aliandika katika hati ya kiapo iliyothibitishwa ya Februari 25, 2015, kwamba "baada ya kuongea, kunywa na kucheza," inadaiwa aliingia kwenye chumba na "Shawn" ili kushikana, akimrejelea rapa huyo kwa jina lake halisi, Shawn Corey Carter.

Kisha akasema, "Shawn na mimi tulifanya mapenzi kwa kutumia kinga lakini kinga ilivunjika."

Satterthwaite pia alibaini katika hati hiyo kwamba alimuona Jay-Z wiki mbili baada ya madai yao ya uhusiano na inasemekana alimtaka "kuondoka" naye.

Hata hivyo, alidai kuwa alimkana rapper huyo wa "Can I Get A .." kwa sababu mama yake "angefadhaika."

"Sikumwona tena hadi miaka kadhaa baadaye kwenye runinga lakini bado sikujua jina lake halisi hadi baadaye na sikujua jinsi ya kumfikia," Satterthwaite alihitimisha katika barua hiyo.

Kulingana na Daily Mail, aliaga dunia mwaka wa 2019 lakini hati yake ya kiapo imeibuka tena kupitia mwanawe anayedaiwa kuwa wa Jay-Z alipokuwa akifuatilia kesi ya ubaba dhidi ya rapper huyo wa "99 Problems".

Rymir Satterthwaite hivi majuzi aliwasilisha amri ya mahakama ikitaka Jay-Z apimwe DNA. Inasemekana amekuwa akipambana kuthibitisha kuwa bilionea huyo ni babake tangu akiwa na umri wa miaka 21 na aliiomba mahakama mwezi Februari kufuta rekodi za mwaka 2012.