logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nimemjua Chioma kwa zaidi ya miaka 20 ni uamuzi bora zaidi niliwahi kufanya - Davido

Davido alisema kuwa anamfahamu Chioma kwa takriban miaka 20 na kwamba yeye ni mpishi bora.

image
na Davis Ojiambo

Burudani23 May 2023 - 07:24

Muhtasari


  • • Hivi majuzi tu, alipotoa albamu yake iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu, “Timeless,” Davido alimwandikia barua ya kugusa moyo mkewe, Chioma.
  • • Mtawala wa 30 BG alirejea muziki wake na kazi bora hii baada ya kutokuwepo kwa muda mrefu.
Davido afunguka jinsi walivyokutana na Chioma akiwa mwaka wake wa kwanza chuoni.

Davido, msanii maarufu kutoka Nigeria, amefichua baadhi ya sababu za ndoa yake na Chioma.

Msanii huyo alijibu swali "Nini ufunguo wa furaha katika kupata mpenzi wako" katika mahojiano na The Beat Atlanta kwa kusema kuwa “ni kuwa na mtu ambaye ulikuwa na raha naye.”

Alidai kuwa yeye na Chioma walikua pamoja kwa kuwa walikuwa wakistarehe mara moja walipokutana kwa mara ya kwanza, katika mwaka wake wa kwanza chuoni.

Davido alidai kuwa Chioma amekuwa sehemu yake na aliwashauri wengine kuchagua mwenzi anayefaa kwa kuwa yeye na mkewe walikuwa muunganiko uliotengenezwa mbinguni.

Davido alisema kuwa anamfahamu Chioma kwa takriban miaka 20 na kwamba yeye ni mpishi bora. Ulikuwa uamuzi bora zaidi kuwahi kufanya, alisema katika hitimisho lake.

“Mapenzi yangu kwa Chioma ni mapya kila siku. Yeye ni sehemu yangu. Nimemjua kwa miaka 20. Yeye ni chaguo na uamuzi sahihi ambao niliwahi kufanya maishani na kama ningeruhusiwa kuoa tena basi nitamuoa mpenzi wangu Chioma,” msanii huyo alisema.

Hivi majuzi tu, alipotoa albamu yake iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu, “Timeless,” Davido alimwandikia barua ya kugusa moyo mkewe, Chioma.

Mtawala wa 30 BG alirejea muziki wake na kazi bora hii baada ya kutokuwepo kwa muda mrefu. Wasanii wa Nigeria na wa kigeni, wakiwemo Asake, Fave, Focalistic, na Angelique Kidjo, wameshirikishwa kwenye albamu hiyo yenye nyimbo 17.

Katikati ya shamrashamra na mbwembwe za mradi huo, Davido alichukua muda mfupi kumuenzi mkewe, Chioma, ambaye amekuwa pembeni yake katika hali ngumu na mbaya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved