logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kennedy Rapudo aeleza jinsi alivyopata na Amber Ray

Rapudo alieleza kwa nini hakupoteza muda wake alipogundua Amber Ray alikuwa single

image
na Davis Ojiambo

Burudani19 June 2024 - 13:26

Muhtasari


  • •Rapudo alieleza kwa nini hakupoteza muda wake alipogundua Amber Ray alikuwa single akisema ni kwa sababu alikuwa kwenye foleni akingoja karibu miaka 2.
  • •Rapundo alieleza kuwa alichukua hatua ya kwanza ya kumsogelea na kuanza mazungumzo ya kumfahamu Amber Ray.
Kennedy Rapudo na mkewe Amber Ray

Mfanyabiashara Mkenya Kennedy Rapudo  amefichua jinsi alivyokutana na sosholaiti Mkenya Amber Ray, ambaye sasa ni mama wa watoto wake.

Akiongea kwenye mahojiano mafupi na Parents Magazine, Rapudo alifunguka na kusema kuwa  alikutana na Amber Ray kwenye ukumbi wa outdoor park and chill.

“Alinikatia, kulikuwa mahali huko Thika road, ambapo watu walienda kuegesha magari, kutuliza, na kunywa.

 Kwa hivyo, nilienda pale nikiwa nimeegesha gari, na ndipo nikagundua kuwa kuna mwanamke ambaye alikuwa akinitazama kwa namna fulani iliyonifanya nitamani kumkaribia.”

Anaendelea kueleza kuwa alichukua hatua ya kwanza ya kumsogelea na kuanza mazungumzo ya kumfahamu.

Walikutana tena, na mara wakaachana na wapenzi wao, wakaanza kuchumbiana.

“Mimi ndiye nilienda huko na kuongea naye, nikikiri kwamba alikuwa mrembo, na nilikuwa nimemuona kwenye mitandao ya kijamii.

Alikua na mtu na mimi nilikua na mtu, the moment alikua single hivi nikaingia mbio.” Kennedy Rapudo alisema.

Rapudo alieleza kwa nini hakupoteza muda wake alipogundua Amber Ray alikuwa single , akisema ni kwa sababu alikuwa kwenye foleni kwa karibu miaka 2.

Zaidi ya hayo, ilikuwa rahisi kumshinda kwa sababu tayari alikuwa ameshajenga hamu ya kuwa naye, jambo ambalo lilikubalika.

“Kwa kweli alikuwa akijaribu kuniunganisha na rafiki yake mmoja, lakini nilipendezwa naye, kwa hivyo siku moja, aliniuliza ikiwa tunaweza kunywa glass of wine, na iliyobaki ni historia.” Kennedy alieleza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved