logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Damu ya Rex haiendi hivo,' Mejja aapa kushiriki maandamano ya Jumanne kupinga mswada wa fedha

Mejja ni miongoni mwa watu mashuhuri wengi wanaokataa waziwazi mswada wa fedha

image

Burudani22 June 2024 - 11:17

Muhtasari


  • Kupitia ukurasa wake wa Instagram, aliandika kwamba hakuweza kujitokeza siku ya Alhamisi kwa sababu ya majukumu ambayo hayangeweza kuepukika na mtoto wake lakini akaahidi kujitokeza Jumanne.
Mejja afichua sababu za wanaume kukwamilia wanawake warembo na wakatili.

Mwanamuziki maarufu wa Genge, Mejja alitangaza kwamba ataungana na vijana katika maandamano yajayo ya kupinga Mswada wa Fedha wa 2024 wenye utata.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, aliandika kwamba hakuweza kujitokeza siku ya Alhamisi kwa sababu ya majukumu ambayo hayangeweza kuepukika na mtoto wake lakini akaahidi kujitokeza Jumanne.

Alisema kuwa uwepo wake utakuwa wa kutoa heshima kwa kijana aliyedaiwa kupigwa risasi na polisi na kuaga dunia, Rex,  Alhamisi jioni alipokuwa akielekea nyumbani baada ya kupinga Mswada wa Fedha.

” Jana sikuweza juu ya mtoi but Tuesday 25th ni kitambi na teargas. Damu ya Rex haiendi hivo RIP ni mgenge na mbogi,” alisema.

Mejja ni miongoni mwa watu mashuhuri wengi wanaokataa waziwazi mswada wa fedha ambao ulilazimishwa kwa Wakenya na serikali inayotawala.

Siku ya Alhamisi, watu mashuhuri wengi wa Kenya, washawishi na waundaji maudhui waliingia barabarani kupinga Mswada wa Fedha.

Watu kadhaa mashuhuri walionekana mitaani huku waiwa wameinua mabango ya kupinga mswada wa fedha.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved