logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mr Ibu kuzikwa Ijumaa miezi 3 baada ya kifo chake

Siku ya Jumapili, Juni 30, kutakuwa na sherehe ya shukrani kwa familia ya mwigizaji.

image

Burudani27 June 2024 - 13:02

Muhtasari


  • "Nina huzuni sana kwamba siko na mume wangu hapa. Sina furaha hata kidogo baada ya juhudi na mateso yote tuliyopitia kuokoa maisha yake,” aliambia Vanguard
Marehemu Mr. Ibu.

Mwigizaji na mchekeshaji wa Nigeria Mr Ibu atazikwa kesho Ijumaa Juni 28 miezi mitatu baada ya kifo chake.

Usiku wa heshima ulifanyika Jumatano katika jimbo la Enugu. Mke wa mwigizaji huyo wa Nollywood alikumbuka taabu alizopitia wakati akitafuta matibabu.

"Nina huzuni sana kwamba siko na mume wangu hapa. Sina furaha hata kidogo baada ya juhudi na mateso yote tuliyopitia kuokoa maisha yake,” aliambia Vanguard

Aliongeza;

“Sijui niseme nini! Nianzie wapi? Inasikitisha sana kuona mume wangu akilia kama mtoto mchanga nami, akisema "Oh darasa la kwanza ni mimi?" Nilikuwa namuangalia mume wangu akilia na kusaga meno. Nilikuwa naye hospitalini.

“Kuna wakati tulitaka kumsafirisha nje ya nchi kwa matibabu zaidi. Tulituma barua kwa hospitali mbili za India, Marekani na Ujerumani, lakini zote zilimkataa," alisema

Leo Alhamisi, Juni 27, kutakuwa na ibada ya Kikristo nyumbani kwa mwigizaji huyo eneo la Eziokwe Amuri, Nkanu Magharibi, Nigeria.

Siku ya Ijumaa, Juni 28, mwigizaji atazikwa.

Siku ya Jumapili, Juni 30, kutakuwa na sherehe ya shukrani kwa familia ya mwigizaji.

Jina halisi John Ikechukwu Okafor alizaliwa tarehe 17 Oktoba 1961 na kufariki tarehe 2 Machi 2024.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved