logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Bora akaunti ya benki iko sawa!” Mulamwah asema baada ya kupoteza akaunti ya TikTok

“Kwa sasa sina akaunti kwenye TikTok, msitapeliwe huko,” aliongeza.

image
na Davis Ojiambo

Burudani03 July 2024 - 07:42

Muhtasari


    Mchekeshaji Mulamwah ni mwathirika mwengine katika msururu wa watu wengi ambao wamekuwa wakipoteza akaunti zao za TikTok katika mazingira yasiyojulikana.

     Mulamwah alichapisha ujumbe akithibitisha kupotea kwa akaunti yake kwenye mtandao huo wa video fupi, katika kile kilichoonekana kama ni kufungiwa.

    Mpaka wakati inatoweka, akaunti ya Mulamwah ilikuwa imejikusanyia jumla ya wafuasi milioni 1.1 na hilo lilionekana kuwa pigo kuu kwa mchekeshaji huyo.

    Hata hivyo, Mulamwah alijitia hamnazo akisema kwamba kwa sasa hana akaunti katika mtandao huo ila anashukuru Mungu akaunti yake ya benki haijaathirika kwa njia yoyote ile.

    “Bora akaunti yangu ya benki ya Equity iko sawa, tunasonga mbele,” Mulamwah alisema.

    Pia alitumia fursa hiyo kuwatahadharisha mashabiki wake kwamba kwa sasa hayuko tena kwenye TikTok na wakuwe macho wasije wakahadaiwa kwani kuna walaghai wengi wameshaanza kufungua akaunti kwa jina lake wakijifanya kuwa yeye.

    “Kwa sasa sina akaunti kwenye TikTok, msitapeliwe huko,” aliongeza.

    Katika miezi ya hivi karibuni, watu wengi wamekuwa wakilia katika mitandao ya kijamii baada ya kufungwa kwa ghafla kwa akaunti zao za TikTok bila kupatiwa sababu.

    Baadhi ya walioonesha kufadhaika kwao baada ya akaunti zao kufungwa ni pamoja na Faustine Baba Talisha ambaye yake ilifungwa saa chache baada ya kufikisha wafuasi milioni moja, Njoki Murira na wengine.


    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved