logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Babu Owino aahidi kumsomesha mwanafunzi aliyeonekana akiuza mahindi usiku

Eric Omondi ameahidi kumsaidia mwanafunzi aliyeonekana akiuza mahindi usiku eneo la Jomoko,barabara kuu ya Thika.

image
na Davis Ojiambo

Burudani05 July 2024 - 09:07

Muhtasari


  • •Msichana huyo alionekana akiuza mahindi akiwa amevalia sare ya shule  kando ya barabara katika eneo la Jomoko, barabara kuu ya Thika 
  • •Tukio hilo lilimfanya Babu Owino kukumbuka enzi zake akiuza pombe aina ya Chang'aa kwa maisha yake yote ya shule ya msingi na ya sekondari.

Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino ameahidi kufadhili masomo ya msichana anayekwenda shule ambaye alirekodiwa akiuza mahindi ya kuchemsha usiku.

Video ya msichana mdogo akiwa amevalia sare ya shule alipokuwa akiuza mahindi kando ya barabara katika eneo la Jomoko kando ya barabara kuu ya Thika ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii mnamo Alhamisi, Julai 4, 2024.

Kupitia ukurasa wake Facebook,Babu Owino mnamo Ijumaa, Julai 5, 2024, aliomba usaidizi wa kumtafuta msichana huyo ili aweze kumfadhili masomo yake na kuwasaidia wazazi wake kuanzisha biashara.

Inasemekana kuwa msichana huyo huondoka katika Shule ya Msingi ya Kisiwa mjini Thika kila jioni kwenda kuuza mahindi hayo kando ya barabara.

Hata hivyo,Babu Owino alisimulia jinsi  tukio hilo lilimkumbusha wakati alipokuwa akiuza pombe aina ya chang’aa kila siku kutoka shuleni kwa maisha yake yote ya shule ya msingi na sekondari.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved