logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sandra Dacha afichua ndoto ya mwanawe ni kukutana na mwanasoka Neymar siku moja

Mwanawe Sandra Dacha kwa sasa ana umri wa miaka 10.

image
na Davis Ojiambo

Burudani08 July 2024 - 06:06

Muhtasari


    Sandra Dacha na mwanawe.

    Mwigizaji Sandra Dacha ni mama mwenye fahari kushuhudia mwanawe akifikisha umri wa miaka 10.

    Dacha alimsherehekea mwanawe wa kiume kwa picha kadhaa kupitia ukurasa wake wa Instagram akiwa amevalia mavazi ya kucheza kandanda pamoja na mpira mkononi.

    Mwigizaji huyo alifichua kwamba mwanawe anapenda sana mchezo wa kandanda na kusema kila siku huwa anazunumzia jinsi anapenda kumtazana mchezaji kutoka Brazili, Neymar Jr akiwa uwanjani.

    Dacha alisema kwamba ndoto ya mwanawe muda wote ni kukutana na mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona na PSG ambaye sasa anakipiga zake Saudi Arabia kwa klabu ya Al Hilal.

    “UPENDO alionao mwanangu kwa mwanasoka huyu wa Brazil aitwaye NEYMAR ni nje ya dunia🤦🏿️🤣 anakunywa na kula kila siku akimtaja😆 na anachotamani ni kuonana naye tu siku fulani😇” Sandra Dacha alifichua.

    Ili kumweka katika mkondo sahihi kutimiza ndoto yake, mwigizaji huyo anayejiita kwa jina la majazi la Biggest Machine alisema mwanawe huwa anafanya mazoezi katika academia moja ya soka.

    “Mapenzi yake kwa soka yalianza tangu zamani alipokuwa na umri wa mwaka mmoja na hapa tulipo sasa, Jeawel anafanya mazoezi na Ballers Of God Football Academy(BOG). Tafadhali nisaidie kumtakia bingwa wa siku zijazo mema,” Dacha alisema.

     


    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved