logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Dem wa Facebook aeleza sababu ya kuwepo kwa kanisa nyumbani kwao

Alisema ni kwa kuwa kwao ni watu wa maombi na kwa sababu hiyo wana kanisa katika kiwanja chao

image
na Davis Ojiambo

Burudani10 July 2024 - 12:53

Muhtasari


  • •Akieleza sababu ya kuwa na kanisa nyumbani kwao alisema ni kwa kuwa kwao ni watu wa maombi na kwa sababu hiyo wana kanisa katika kiwanja chao.
  • •Pia Dem Wa Facebook alionyesha nyumba anayowajengea wazazi wake, nymba wa vyumba 3 vya kulala.

Mtayarishaji wa maudhui na mcheshi wa Kenya Dem Wa Facebook, kupitia chaneli yake ya YouTube, aliamua kuwafahamisha mashabiki wake kwa nini kuna kanisa nyumbani kwao.

Dem Wa Facebook ambaye aliyasema hayo alipokuwa akiwapa mashabiki wake ziara nyumbani kwao.

Pia alionyesha vyumba 3 vya kulala aliyokuwa akijegea wazazi wake.

Akieleza sababu ya kuwa na kanisa nyumbani kwao alisema ni kwa kuwa kwao ni watu wa maombi na kwa sababu hiyo wana kanisa katika kiwanja chao.

“Hiyo ni church, my dad, alijenga kwa boma. Sisi tunakuanga watu wa maombi 24-7, hapa kwetu kunakuanga na sheria za maombi.” Dem wa Facebook alisema huku akionyesha kanisa kwa mbali.

Anaendelea kueleza kuwa awali walikuwa wakitumia nyumba yao kama sehemu ya ibada hadi Watoto.

Hivyo Dem Wa Facebook na ndugu wengine walimshauri baba yao kufikiria kujenga nyumba tofauti ambayo inaweza kutumika.

“Tulisema hatuombei kwa nyumba, tunahitaji kuwa serious na maombi. Hiyo ni kanisa la familia yetu hata vile nimekuja lazima tuombe tusome verse, there’s power in prayer.” Dem wa facebook alisema.

Hata hivyo, Dem Wa Facebook alieleza kwamba alikuwa na wakati mgumu kujaribu kulala kwani hakuwa kwa dini kabisa kama vile wazazi wake walivyokuwa, lakini aliahidi kufuata nyayo za baba yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved