Mwigizaji Nyaboke Moraa apoteza bintiye kifungua mimba,Marrie Achieng

Kifo cha Achieng kinakuja zaidi ya mwezi mmoja baada ya mwigizaji Nyaboke kumpoteza kakake.

Muhtasari

•Mwigizaji Nyaboke Moraa amepoteza bintiye Marrie Achieng,ambaye alikuwa kifungua mimba.

•Taarifa hii ilithibitishwa na mwigizaji Sandra Dacha kupitia ukurasa wake wa Instagram Julai 28,2024.

Mwigizaji Nyaboke Moraa na bintiye Marrie Achieng
Mwigizaji Nyaboke Moraa na bintiye Marrie Achieng
Image: instagram

Mwigizaji na mtayarishaji maudhui maarufu nchini Kenya Nyaboke Moraa, ameingia katika majonzi kufuatia kifo cha bintiye, Marrie Achieng.

Kifo cha Marrie kiliwekwa wazi na mwigizaji Sandra Dacha.

"Ni kwa masikitiko makubwa ninakutangazia kifo cha binti wa @nyabokemoraa. Maombi yako ndiyo anayohitaji kwa sasa🙏🏿 REST IN PEACE Marrie😭,” ilisoma chapisho kutoka kwa Sandra Dacha.

Chanzo cha kifo cha Marrie bado hakijawekwa wazi.

Kifo cha Achieng kinakuja zaidi ya mwezi mmoja baada ya mwigizaji Nyaboke kumpoteza kakake.

"Dakika moja tunafurahi na kufurahiya, dakika inayofuata tunapotea. Familia ya Nyariki imepigwa tena. Tumempoteza kaka yetu mkubwa. Tulisubiri uje kwa mkutano wetu lakini ulikosa safari yako ya ndege. Sasa tunaomboleza kifo chako cha ghafla.....hizi sasa hata ni gani hazieleweki???hatutapumua hii mwaka jameni katika familia yetu? Sigh, "alishiriki  mnamo Juni 10, 2024

Mashabiki na watu mashuhuri ambao wameomboleza bintiye Nyaboke:

nanaowiti ;OmG! Nooooooooooooooo!! Nooooooo!!!!! 💔💔💔💔💔

nycewanjeri; Ooooh Nooooo 😭😭😭💔💔 Mungu ampe amani 🕊️

aggie_the_dance_queen ;Ooh no.Mungu ampe amani na familia yake🕊️🙏🏾

mwendemacharia; Oooo nooo..tukimuombea yeye na familia. Rambirambi zangu za dhati