logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wema Sepetu akerwa na waislamu wenzake mfungo huu wa ramadhani

Sepetu amesema hajawahi kuona kwamba kumutakia mtu heri njema ya kuzaliwa ni kosa wakati wa mfungo wa Ramadhani.

image
na Japheth Nyongesa

Mastaa wako11 March 2025 - 12:40

Muhtasari


  • Muigizaji maarufu Wema Isaac Sepetu ameonesha kukerwa na baadhi ya waislamu wenzake hasa wale wanaotumia mitandao ya kijamii ambao hawakufurahishwa na kitendo chake cha kumutakia mpenziwe heri njema ya kuzaliwa.
  • Mwanadada huyo pia alifichua kwamba hana hamu sana na ndoa. "Ndoa sio kitu ambacho mimi nakiona au nakiota, na sio kitu ambacho labda nakitamani.

Muigizaji maarufu Wema ISepetu ameonesha kukerwa na baadhi ya waislamu wenzake hasa wale wanaotumia mitandao ya kijamii ambao hawakufurahishwa na kitendo chake cha kumutakia mpenziwe heri njema ya kuzaliwa.

Wema Sepetu ambaye aliwajibu kupitia njia ya Vdeo amesisitiza kwamba hajawahi kuona kwamba kumutakia mtu heri njema ya kuzaliwa ni kosa wakati wa mfungo wa Ramadhani.

"Yote tisa waislamu wa mitandaoni tutashindwa kuishi maisha yetu walahi. Kwa hivyo hata mtu akimutakia mwingine heri njema ya kuzaliwa ni makosa. Tunaambiwa Ramadhani iko, kwani Ramadhani ikiwa Hakuna kuwishi mtu Happy Birthday. Mbona maajabu. Mimi sijawahi kuona au labda mimi ndio sijui. Msifanye ivyo mnakosea,"alisema muigizaji Wema Sepetu.

Mwanadada huyo pia amefunguka kwamba hangependa mtu kuingilia mapenzi yake na mpenziwe hii ni baada ya fununu kuenea kwamba mama yake mzazi hampendi kabisa mpeniziwe Whozu ambaye ni mwanamziki kutoka katika taifa hilo la Tanzania.

Amesisitiza kwamba mahusiano hayo hayafai kuingiliwa na mtu yeyote maana ni yake na hakuna mtu ambaye anafaa kumchagulia mtu wa kupenda.

'"Mimi nasema kwamba maisha yangu mimi ya mapenzi hayamuhusu mtu yeyote hata wewe. Yananihusu mimi na mpenzi wangu. Hayatakiwi kumuhusu mtu yeyote mwingine hata kama hapendi, bora mimi na mpenzi wangu tuko sawa. sijui kama niko sahihi au hapana. Ninachojua ni kwamba mama hana shida, yuko sawa lakini hili linakwenda kwa mutu yeyote huko inje," aliweka wazi Sepetu.

Muigizaji huyo maarufu na mshindi wa tuzo ya miss Tanzania pia amefunguka kwamba yeye anamzidi Mpenziwe Whozu kwa umri wa miaka sita na wamekuwa pamoja kwa zaidi ya miaka minne kufikia sasa.

'Namuzidi na mika sita, nimemzidi Whozu na miaka sita na mimi naona siyo mibaya sana, hata kama ingekuwa 10 kwani shda iko wapi, kuna watu wanashindaniana miaka 20 sembuse mimi miaka sita. Huu mwaka wa nne wa 'mapenzi' na tupo.," alikiri.

Mwanadada huyo pia alifichua kwamba hana hamu sana na ndoa. "Ndoa sio kitu ambacho mimi nakiona au nakiota, na sio kitu ambacho labda nakitamani. Nadhani imeniharibu kimawazo hasa kutokana na watu wangu wa karibu," aliweka wazi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved