Kaptura ama shorts ni vazi ambalo wanawake wamekuwa wakivalia aidha wakiwa nyumbani ama kwa shughuli zao za kawaida japo si wote wakivalia vazi hilo huvutia pakubwa.
Hapa nimekuandalia baadhi ya watu maarufu nchini ambao wakivalia kaptura huwaacha akina Wanyonyi ,Wafula ,Omondi na wengine Mijulus yao ikiwa imesimama tisti, Tazama.
1.Talia Oyando
Talia Oyando ni mtangazaji. Kando na utangazaji wake, kichuna huyu anapenda sana kuvalia Kaptura akiwa hata kazini ama kwa shughuli nyinginezo.
Jacky Vike
Awinja kama anavyofahamika sana na wengi ,anapenda zaidi kuvalia kaptura ambayo kutokana na urefu wa mikuu yake na kiuno kilichokubalika, huwaacha akina yahe wakiwa vinywa wazi.
Kush Tracey
Msanii huyu ana mazoea ya kuwaumiza wanaume hisia zao kutokana na tabia yake ya kuvalia kaptura kila anapokuwa anajumuika na watu katika hafla mbalimbali.
Avril
Ni msanii anayefahamika na wengi kutokana na umbo lake la kuvutia. Avril kama wengine tu akivalia kaptura huibua gumzo haswa miongoni mwa wanaume ambao huvutiwa sana na urembo.
Brenda Wairimu
Licha ya kuwa na miaka 30, Brenda ni miongoni mwa wanawake maarufu nchini ambao hupenda zaidi kuvalia kaptura katika hafla tofauti na hata wakati wa kuigiza vipindi mbalimbali.
Wanjiku Mburu
Anajulikana sana kama Mama Baha katika kipindi cha Machachari nchini. Tazama jinsi toto hili linapotokea likivalia kaptura.
Je wafahamu baadhi ya watu wengine nchini ambao wakivalia kaptura mwonekano wao huwa wa kuvutia? Tuchapie Gumzo.