CHAN: Mike Kibwage yupo tayari kuwabwaga washambulizi

Nahodha wa KCB Michael Kibwage amesema kuwa yupo tayari kupigania nafasi yake kwenye kikosi cha kwanza cha Harambee stars kitakacho shiriki mechi ya kufuzu michuano ya Chan dhidi ya Tanzania siku ya Jumapili.

Kibwage anatarajia ushindani mkubwa kutoka kwa Joash Onyango wa Gor Mahia Pamoja na Bernad ochieng kutoka Wazito Fc.

Kibwage, Mwenye umri wa miaka 21 aliitwa kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha stars na Kocha Sebastiane Migne mwaka uliopita kuiwakilisha Kenya kwenye mechi za Intercontinetal kule nchini india.

"Sasa ni wakati wa kumlipa kocha wangu kwa kuniamini na kunipa nafasi hii ya kuliwakilisha taifa letu. Cjapata nafasi ya kucheza kwenye timu ya taifa ila sasa ni wakati wanNahodha wa KCB Michael Kibwage amesema kuwa yupo tayari kupigania nafasi yake kwenye kikosi cha kwanza cha Harambee stars kitakacho shiriki mechi ya kufuzu michuano ya Chan dhidi ya Tanzania siku ya Jumapili. gu wa kumwonyesha kocha kuwa ninao uwezo wa kufanya makubwa kwenye kikosi cha kwanza cha taifa." Kibwage alisema

Awali, Kibwage alichezea AFC misimu miwili kabla ya kwenda zake KCB kwa ajili ya kupata dakika nyingi uwanjani.

Kulingana naye Mike, Harambee Stars inayo nafasi kubwa ya kupenye kwenye hatua ya makundi ya michuano ya CHAN na hata uwezo wa kulishida taji hilo.

Michuano ya CHAN huchezwa na wachezaji wanaocheza barani Africa peke yao.