Chelsea yapania kuwapiga mnada wachezaji 11

EZ16-77WkAEoUCj.jfif
EZ16-77WkAEoUCj.jfif
Chelsea wanaripotiwa kuwa tayari kuwaondoa wachezaji wao 11 msimu huu ambapo itakuwa historia katika klabu hiyo ya Uingereza.

Chelsea wanapania kuimarisha kikosi chao msimu ujao na wachezaji kama vile Pedro, Jorginho na Barkley wanatazamiwa kuondoka Stamford Bridge.

Tayari Blues wako katika mchakato wa kumsajili Timo Werner kutoka Leipzig ambaye anatazamiwa kutia saini mkataba wa miaka mitano na wenyeji hao wa London.

Meneja wa Blues, Frank Lampard tayari amechomoa pauni 38 milioni kumpata winga wa Ajax Hakim Ziyech ambaye alitia saini mkataba mwezi Januari.

Miongoni mwa wachezaji ambao wanatazamiwa kuondoka Chelsea msimu huu ni winga Mbrazil, Willian ambaye anaweza kusalia Uingereza ama aondoke na kuyoyomea katika Ligi ya Uhispania ya La Liga.

Michy Batshuayi pia ni mchezaji mwingine aliyetupwa sokoni huku Newcastle na Crystal Palace wakiaminika kuwa makini kumsajili Mbelgiji huyo.

Inaaminika Frank Lampard anamumezea mate mchezaji wa Leicester, Ben Chilwell na fowadi mwenye miaka 23 wa Sassuolo, Jeremie Boga, ambaye alikuwa Stamford Bridge kwa miaka tisa kabla ya kujiunga na klabu yake ya sasa miaka miwili iliyopita.

Kinyume na Boga ambaye Blues wanampendelea, pia watalazimika kugharamika zaidi kumpata Chilwell, Lampard akipania kuhimarisha safu ya ulinzi.

Hata hivyo, lengo la sasa la Chelsea msimu huu ni kumaliza mingoni mwa vilabu nne bora ambapo ufanisi huo utawawezesha kushiriki katika mashindano ya Mabingwa wa Ligi msimu ujao.