Chuo kikuu cha Nairobi hakitafunguliwa Septemba baada ya wafanyikzi 3 kupatikana na Covid 19

UON
UON
Chuo kikuu cha Nairobi kimefutilia mbali mipango ya kurejelea shughuli zake  septemba  baada ya wafanyikazi wake watatu kupatikana na virusi vya corona .

Uamuzi huo umeafikiwa na senate ya chuo hicho baada ya kufanya mkutano siku ya jumatano  .Naibu mhadhiri huu wa chuo hicho Stephen Kiama amesema senate sasa itatoa tarehe mpya za kufunguliwa taasisi hiyo . Mojawapo ya kinachoweza kuamuliwa ni kufunguliwa kwa chuo hicho katikati ya mwezi novemba  endapo visa vya coronavirus nchini vitapungua .

Hata hivyo Kiama amesema  mafunzo na masomo yataendelea kupitia nia za mitandao  na hakuna  mwanafunzi anayefaa kuhitimu mwaka huu  atakosa kufanya hivyo . Waziri wa elimu George Magoha  mwezi juni alikuwa ametangaza kwamba  shule zitafunguliwa januari mwakani .hata hivyo  kufunguliwa kwa taasisi za elimu ya juu kulitarajia kutegemwa kupungua kwa visa vya ugonjwa huo  nchini .