Covid-19: Idadi ya waliofariki kote duniani yazidi milioni 1

corona
corona
 Idadi ya watu kote duniani walioaga dunia kwa ajili ya covid 19  imepita watu ilioni moja  watafiti wanasema  huku sehemu nyingi zikizidi kuripoti visa Zaidi vya  maambukizi

Takwimu zilizotolewa na chuo kikuu cha  Johns Hopkins  zinaonyesha kwamba vifo katika mataifa ya Marekani ,Brazil  na India vinajumuisha nusu ya vifo vyote duniani .

Wataalam wanaonya kwamba idadi kamili huenda iko juu Zaidi .katibu mkuu wa umoja wa mataifa  António Guterres amesema  idadi hio ni kuhofisha

" Walioaga dunia walikuwa baba ,mama ,dada ,kaka wake na waume ,marafiki na wenzuru . uchungu wa kuwapoteza umezidishwa na  makali ya janga hili’ amesema Guterres

Hatua hiyo imejiri miezi kumi tangu ugonjwa huo kulipukia nchini China katika mkoa wa Wuhan .

Janga hilo limesambaa hadi katika mataifa 188  huku visa milioni 32 vikithibitishwa . hatua za kuzuia maambukizi Zaidi kama vile marufuku za kutotoka nje na kutosafiri zimesababisha chumi za mataifa mengi kudhoofika .

Kwingineko juhudi za kutafuta chanjo dhidi ya coronavirus zinaendelea  ingawaje shirika la afya duniani WHO  limesema kwamba ugonjwa huo huenda ukasababisha vifo vya watu miliopni 2 kabla ya chanjo kamili kupatikana .

Marekani ndio yenye idadi kubwa ya watu walioaga dunia  baada ya watu Zaidi ya 205,000 kuangamia  ikifuatwa na Brazil ikiwa na watu 141,700 kisha india ni ya tatu kwa  vifo 95,000