COVID-19: Kenya Kutenga fedha kwa wiki moja kabla ya kuachiliwa kwa matumzi kuzuia usambaaji wa Corona

Benki kuu ya Kenya  itazitenga pesa mpya kwa wiki moja  kabla ya kuiachiliwa katika mfumo wa matumizi ili kukabiliana na usambaaji wa virusi vya Corona .

Akizungumza  kuhusu mikakati iliyochukuliwa na sekta ya kifedha kupambana na usambaaji wa virusi hivyo  gavana wa benki kuu Patrick Njoroge  amewarai wananchi kutumia fursa ya kuondolewa kwa ada za kutuma pesa za malipo wanapofanya ununuzi badala ya kutumia pesa taslimu.  Sekta ya beki imekubali kulegeza mashari kuhusu mikopo hasa iliyochukuliwa na watu binafsi  kuhakikisha kwamba watu wanamudu kugharamia mahitaji yao ya kila siku .

'' Mikopo yote ya Benki  iliyokuwepo machi tarehe mbili itaweza kuongezwa muda wa malipo hadi mwaka mmoja . wafanyibiashara wadogo wadogo na mashirika yanaweza kuzungumza na benki zao kuhusu kuongezwa muda wa malipo  kulingana na Njoroge .

“ Pia tumezitaka benki zetu  kuodnoa ada za kufahamu masalio ya pesa katika kaunti  na hawafai kutoza malipo yanayotekelezwa kutumia kumbi za simu za mkononi’ ameongeza Njoroge .

Mwenyekiti wa muungano wa wanabenki wa Kenya na maneja mkurugenzi mkuu wa benki ya KCB Joshua Oigara amekariri kujitolea kwa sekta ya benki kuwasaidia wakenya kukabiliana na virusi vya COVID 19  nchini