Covid 19 Survivors: Wafahamu Baadhi ya watu waliopona Virusi vya Corona

Virusi vya Corona vimesababisha  msukosuko mkubwa kote duniani huku nyanja zote zikiathiriwa na kila  upeo wa maisha ya  binadamu ukitikiswa. Licha ya maafa ya watu  zaidi ya  48,000 kote duniani ,  zaidi ta watu laki mbili wamepona ugonjwa huo . Hii hapa orodha  ya watu unaowajua ambao wamepona virusi vya Corona

 Brenda Cherotich na  Brian

Brenda Cherotich na Brian  ni miongoni mwa watu  watatu nchini Kenya ambao wamepona virusi vya Corona .Wawili hao siku ya  Jumatano walizungumza na rais Uhuru Kenyatta kupitia njia ya video na kulitangazia taifa jinsi walivyojipata na virusi hivyo na muda wao katika karantini. Brenda alieleza jinsi ugonjwa huo unavyoweza kukabiliwa na kuwahimiza wakenya walio na daalili za virusi vya Corona kuwa na ujasiri wa kujitokeza mapema ili kupata usaidizi wa matibabu .

Mwana FA

Mwanamuziki huyo wa  bongo aliwashangaza  mashabiki wake kwa kutangaza kupitia instagram kwamba alikuwa amepatikana na virusi vya Corona . Alijitega katika karanti kwa muda alioshauriwa na madaktari na baadaye akatangaza kupona . Waziri wa Afya wa Tanzania Ummy Mwalimu  alithibitisha kwamba Mwana FA ndiye aliyekuwa mgonjwa wa kwanza nchini humo kupona virusi vya COVID 19 .

 Salaam SK

Maneja huyo  wa msanii wa Bongo Diamond Platinumz  alikuwa  miongoni mwa watu mashuhuri waliopatikana na virusi vya Covid 19 . Tangazo kwamba Salaam  alikuwa na virusi  hivyo lilimpelekea Diamond pia kuingia karantini  ili kujitenga na uwezekano wa kuambukizwa. Baadaye hata hivyo Salaama aliibuka na habari njema kwamba ameweza kupona virusi vya Corona .