COVID 19: Visa vya walio na virusi vya corona sasa ni 183 na kufikisha 8,250

corona
corona
Visa vya walio na virusi vya corona  sasa ni    183 na kufikisha jumla ya watu 8,250   walio na ugonjwa huo nchini

Kenya  leo imesajili visa 183 vya virusi vya corona  na kufikisha  visa hivyo kuwa 8,250  katika saa 24 zilizopita. Matokeo hayo ni kutoka sampuli  2,061  amesema waziri wa afya Mutahi Kagwe.

Kutoka visa hivyo 177 ni vya wakenya ilhali sita ni vya raia wa kigeni . watu 119 ni wanaume ilhali 64 ni wanawake huku mtu mwenye umri wa chini sasa  akiwa na umri wa miaka minne  na aliye na umri wa juu zaidi  akiwa na umri wa miaka 64 .

Nairobi inaongoza  kwa visa 100  ,machakos ikiwa na visa 37 ,kiambu ina visa 14 ,Mombasa ina visa 13  ,Kajiado visa 11 ,Nakuru visa 5 na Busia ina visa 3.

Wagonjwa 90 wameruhusiwa kwenda nyumbani  na kufikisha 2504 watu waliopona ugonjwa huo  huku watu watatu wakiaga dunia na kufikisha  167 waliofariki kutokana na ugonjwa huo .

Waziri Kagwe amewaonya wakenya dhidi ya kuwa watepetevu  hasa baada ya rais Uhuru Kenyatta kufungua usafiri  kutoka  kaunti moja hadi nyingine .

Rais Kenyatta hata hivyo  alizidisha muda wa kafyu kwa siku 30 zaidi .